Swahili
Sorah Al-Fajr ( The Dawn )

Verses Number 30

وَالْفَجْرِSorah Al-Fajr ( The Dawn ) Verse Number 1
Naapa kwa alfajiri,
وَلَيَالٍ عَشْرٍSorah Al-Fajr ( The Dawn ) Verse Number 2
Na kwa masiku kumi,
وَالشَّفْعِ وَالْوَتْرِSorah Al-Fajr ( The Dawn ) Verse Number 3
Na kwa viwili viwili na kimoja kimoja,
وَاللَّيْلِ إِذَا يَسْرِSorah Al-Fajr ( The Dawn ) Verse Number 4
Na kwa usiku unapo pita,
هَلْ فِي ذَلِكَ قَسَمٌ لِّذِي حِجْرٍSorah Al-Fajr ( The Dawn ) Verse Number 5
Je! Hapana katika haya kiapo kwa mwenye akili?
أَلَمْ تَرَ كَيْفَ فَعَلَ رَبُّكَ بِعَادٍSorah Al-Fajr ( The Dawn ) Verse Number 6
Kwani hukuona jinsi Mola wako Mlezi alivyo wafanya kina A'di?
إِرَمَ ذَاتِ الْعِمَادِSorah Al-Fajr ( The Dawn ) Verse Number 7
Wa Iram, wenye majumba marefu?
الَّتِي لَمْ يُخْلَقْ مِثْلُهَا فِي الْبِلادِSorah Al-Fajr ( The Dawn ) Verse Number 8
Ambao haukuumbwa mfano wake katika nchi?
وَثَمُودَ الَّذِينَ جَابُوا الصَّخْرَ بِالْوَادِSorah Al-Fajr ( The Dawn ) Verse Number 9
Na Thamudi walio chonga majabali huko bondeni?
وَفِرْعَوْنَ ذِي الأَوْتَادِSorah Al-Fajr ( The Dawn ) Verse Number 10
Na Firauni mwenye vigingi?
الَّذِينَ طَغَوْا فِي الْبِلادِSorah Al-Fajr ( The Dawn ) Verse Number 11
Ambao walifanya jeuri katika nchi?
فَأَكْثَرُوا فِيهَا الْفَسَادَSorah Al-Fajr ( The Dawn ) Verse Number 12
Wakakithirisha humo ufisadi?
فَصَبَّ عَلَيْهِمْ رَبُّكَ سَوْطَ عَذَابٍSorah Al-Fajr ( The Dawn ) Verse Number 13
Basi Mola wako Mlezi aliwapiga mjeledi wa adhabu.
إِنَّ رَبَّكَ لَبِالْمِرْصَادِSorah Al-Fajr ( The Dawn ) Verse Number 14
Hakika Mola wako Mlezi yupo kwenye mavizio anawavizia.
فَأَمَّا الإِنسَانُ إِذَا مَا ابْتَلاهُ رَبُّهُ فَأَكْرَمَهُ وَنَعَّمَهُ فَيَقُولُ رَبِّي أَكْرَمَنِSorah Al-Fajr ( The Dawn ) Verse Number 15
Ama mtu anapo jaribiwa na Mola wake Mlezi, akamkirimu na akamneemesha, husema: Mola wangu Mlezi amenikirimu!
وَأَمَّا إِذَا مَا ابْتَلاهُ فَقَدَرَ عَلَيْهِ رِزْقَهُ فَيَقُولُ رَبِّي أَهَانَنِSorah Al-Fajr ( The Dawn ) Verse Number 16
Na ama anapo mjaribu akampunguzia riziki yake, husema: Mola wangu Mlezi amenitia unyonge!
كَلاَّ بَل لّا تُكْرِمُونَ الْيَتِيمَSorah Al-Fajr ( The Dawn ) Verse Number 17
Sivyo hivyo! Bali nyinyi hamuwakirimu mayatima,
وَلا تَحَاضُّونَ عَلَى طَعَامِ الْمِسْكِينِSorah Al-Fajr ( The Dawn ) Verse Number 18
Wala hamhimizani kulisha masikini;
وَتَأْكُلُونَ التُّرَاثَ أَكْلا لَّمًّاSorah Al-Fajr ( The Dawn ) Verse Number 19
Na mnakula urithi kwa ulaji wa pupa,
وَتُحِبُّونَ الْمَالَ حُبًّا جَمًّاSorah Al-Fajr ( The Dawn ) Verse Number 20
Na mnapenda mali pendo la kupita kiasi.
كَلاَّ إِذَا دُكَّتِ الأَرْضُ دَكًّا دَكًّاSorah Al-Fajr ( The Dawn ) Verse Number 21
Sivyo hivyo! Itakapo vunjwa ardhi vipande vipande,
وَجَاءَ رَبُّكَ وَالْمَلَكُ صَفًّا صَفًّاSorah Al-Fajr ( The Dawn ) Verse Number 22
Na akaja Mola wako Mlezi na Malaika safu safu,
وَجِيءَ يَوْمَئِذٍ بِجَهَنَّمَ يَوْمَئِذٍ يَتَذَكَّرُ الإِنسَانُ وَأَنَّى لَهُ الذِّكْرَىSorah Al-Fajr ( The Dawn ) Verse Number 23
Na ikaletwa Jahannamu siku hiyo, siku hiyo mtu atakumbuka! Lakini kukumbuka huko kutamfaa nini?
يَقُولُ يَا لَيْتَنِي قَدَّمْتُ لِحَيَاتِيSorah Al-Fajr ( The Dawn ) Verse Number 24
Atasema: Laiti ningeli jitangulizia kwa uhai wangu!
فَيَوْمَئِذٍ لّا يُعَذِّبُ عَذَابَهُ أَحَدٌSorah Al-Fajr ( The Dawn ) Verse Number 25
Basi siku hiyo hataadhibu yeyote namna ya kuadhibu kwake.
وَلا يُوثِقُ وَثَاقَهُ أَحَدٌSorah Al-Fajr ( The Dawn ) Verse Number 26
Wala hatafunga yeyote kama kufunga kwake.
يَا أَيَّتُهَا النَّفْسُ الْمُطْمَئِنَّةُSorah Al-Fajr ( The Dawn ) Verse Number 27
Ewe nafsi iliyo tua!
ارْجِعِي إِلَى رَبِّكِ رَاضِيَةً مَّرْضِيَّةًSorah Al-Fajr ( The Dawn ) Verse Number 28
Rejea kwa Mola wako Mlezi umeridhika, na umemridhisha.
فَادْخُلِي فِي عِبَادِيSorah Al-Fajr ( The Dawn ) Verse Number 29
Basi ingia miongoni mwa waja wangu,
وَادْخُلِي جَنَّتِيSorah Al-Fajr ( The Dawn ) Verse Number 30
Na ingia katika Pepo yangu.