Swahili
Sorah Al-Mutaffifin (Those Who Deal in Fraud)

Verses Number 36

وَيْلٌ لِّلْمُطَفِّفِينَSorah Al-Mutaffifin (Those Who Deal in Fraud) Verse Number 1
Ole wao hao wapunjao!
الَّذِينَ إِذَا اكْتَالُواْ عَلَى النَّاسِ يَسْتَوْفُونَSorah Al-Mutaffifin (Those Who Deal in Fraud) Verse Number 2
Ambao wanapo jipimia kwa watu hudai watimiziwe.
وَإِذَا كَالُوهُمْ أَو وَّزَنُوهُمْ يُخْسِرُونَSorah Al-Mutaffifin (Those Who Deal in Fraud) Verse Number 3
Na wao wanapo wapimia watu kwa kipimo au mizani hupunguza.
أَلا يَظُنُّ أُوْلَئِكَ أَنَّهُم مَّبْعُوثُونَSorah Al-Mutaffifin (Those Who Deal in Fraud) Verse Number 4
Kwani hawadhani hao kwamba watafufuliwa
لِيَوْمٍ عَظِيمٍSorah Al-Mutaffifin (Those Who Deal in Fraud) Verse Number 5
Katika Siku iliyo kuu,
يَوْمَ يَقُومُ النَّاسُ لِرَبِّ الْعَالَمِينَSorah Al-Mutaffifin (Those Who Deal in Fraud) Verse Number 6
Siku watapo msimamia watu Mola Mlezi wa walimwengu wote?
كَلاَّ إِنَّ كِتَابَ الْفُجَّارِ لَفِي سِجِّينٍSorah Al-Mutaffifin (Those Who Deal in Fraud) Verse Number 7
Hasha! Hakika maandiko ya wakosefu bila ya shaka yamo katika Sijjin.
وَمَا أَدْرَاكَ مَا سِجِّينٌSorah Al-Mutaffifin (Those Who Deal in Fraud) Verse Number 8
Unajua nini Sijjin?
كِتَابٌ مَّرْقُومٌSorah Al-Mutaffifin (Those Who Deal in Fraud) Verse Number 9
Kitabu kilicho andikwa.
وَيْلٌ يَوْمَئِذٍ لِّلْمُكَذِّبِينَSorah Al-Mutaffifin (Those Who Deal in Fraud) Verse Number 10
Ole wao siku hiyo kwa wanao kadhibisha!
الَّذِينَ يُكَذِّبُونَ بِيَوْمِ الدِّينِSorah Al-Mutaffifin (Those Who Deal in Fraud) Verse Number 11
Ambao wanaikadhibisha Siku ya Malipo.
وَمَا يُكَذِّبُ بِهِ إِلاَّ كُلُّ مُعْتَدٍ أَثِيمٍSorah Al-Mutaffifin (Those Who Deal in Fraud) Verse Number 12
Wala haikadhibishi ila kila mwenye kuruka mipaka, mwenye dhambi.
إِذَا تُتْلَى عَلَيْهِ آيَاتُنَا قَالَ أَسَاطِيرُ الأَوَّلِينَSorah Al-Mutaffifin (Those Who Deal in Fraud) Verse Number 13
Anapo somewa Aya zetu husema: Ni visa vya watu wa kale!
كَلاَّ بَلْ رَانَ عَلَى قُلُوبِهِم مَّا كَانُوا يَكْسِبُونَSorah Al-Mutaffifin (Those Who Deal in Fraud) Verse Number 14
Hasha! Bali yametia kutu juu ya nyoyo zao hao walio kuwa wakiyachuma.
كَلاَّ إِنَّهُمْ عَن رَّبِّهِمْ يَوْمَئِذٍ لَّمَحْجُوبُونَSorah Al-Mutaffifin (Those Who Deal in Fraud) Verse Number 15
Hasha! Hakika hao siku hiyo bila ya shaka watazuiliwa na neema za Mola wao Mlezi.
ثُمَّ إِنَّهُمْ لَصَالُوا الْجَحِيمِSorah Al-Mutaffifin (Those Who Deal in Fraud) Verse Number 16
Kisha wataingia Motoni!
ثُمَّ يُقَالُ هَذَا الَّذِي كُنتُم بِهِ تُكَذِّبُونَSorah Al-Mutaffifin (Those Who Deal in Fraud) Verse Number 17
Kisha waambiwe: Haya ndiyo mliyo kuwa mkiyakadhabisha.
كَلاَّ إِنَّ كِتَابَ الأَبْرَارِ لَفِي عِلِّيِّينَSorah Al-Mutaffifin (Those Who Deal in Fraud) Verse Number 18
Hasha! Hakika maandiko ya watu wema bila ya shaka yamo katika I'liyyin.
وَمَا أَدْرَاكَ مَا عِلِّيُّونَSorah Al-Mutaffifin (Those Who Deal in Fraud) Verse Number 19
Na nini kitakacho kujuvya nini I'liyyin?
كِتَابٌ مَّرْقُومٌSorah Al-Mutaffifin (Those Who Deal in Fraud) Verse Number 20
Kitabu kilicho andikwa.
يَشْهَدُهُ الْمُقَرَّبُونَSorah Al-Mutaffifin (Those Who Deal in Fraud) Verse Number 21
Wanakishuhudia walio karibishwa.
إِنَّ الأَبْرَارَ لَفِي نَعِيمٍSorah Al-Mutaffifin (Those Who Deal in Fraud) Verse Number 22
Hakika watu wema bila ya shaka watakuwa katika neema.
عَلَى الأَرَائِكِ يَنظُرُونَSorah Al-Mutaffifin (Those Who Deal in Fraud) Verse Number 23
Wakae juu ya viti vya enzi wakiangalia.
تَعْرِفُ فِي وُجُوهِهِمْ نَضْرَةَ النَّعِيمِSorah Al-Mutaffifin (Those Who Deal in Fraud) Verse Number 24
Utatambua katika nyuso zao mng'aro wa neema,
يُسْقَوْنَ مِن رَّحِيقٍ مَّخْتُومٍSorah Al-Mutaffifin (Those Who Deal in Fraud) Verse Number 25
Watanyweshwa kinywaji safi kiliyo tiwa muhuri,
خِتَامُهُ مِسْكٌ وَفِي ذَلِكَ فَلْيَتَنَافَسِ الْمُتَنَافِسُونَSorah Al-Mutaffifin (Those Who Deal in Fraud) Verse Number 26
Muhuri wake ni miski. Na katika hayo washindanie wenye kushindana.
وَمِزَاجُهُ مِن تَسْنِيمٍSorah Al-Mutaffifin (Those Who Deal in Fraud) Verse Number 27
Na mchanganyiko wake ni Tasniim,
عَيْنًا يَشْرَبُ بِهَا الْمُقَرَّبُونَSorah Al-Mutaffifin (Those Who Deal in Fraud) Verse Number 28
Chemchem watakayo inywa walio kurubishwa.
إِنَّ الَّذِينَ أَجْرَمُوا كَانُواْ مِنَ الَّذِينَ آمَنُوا يَضْحَكُونَSorah Al-Mutaffifin (Those Who Deal in Fraud) Verse Number 29
Kwa hakika wale walio kuwa wakosefu walikuwa wakiwacheka walio amini.
وَإِذَا مَرُّواْ بِهِمْ يَتَغَامَزُونَSorah Al-Mutaffifin (Those Who Deal in Fraud) Verse Number 30
Na wanapo pita karibu yao wakikonyezana.
وَإِذَا انقَلَبُواْ إِلَى أَهْلِهِمُ انقَلَبُواْ فَكِهِينَSorah Al-Mutaffifin (Those Who Deal in Fraud) Verse Number 31
Na wanapo rudi kwa watu wao hurudi nao wamefurahi.
وَإِذَا رَأَوْهُمْ قَالُوا إِنَّ هَؤُلاء لَضَالُّونَSorah Al-Mutaffifin (Those Who Deal in Fraud) Verse Number 32
Na wanapo waona husema: Hakika hawa ndio khasa walio potea.
وَمَا أُرْسِلُوا عَلَيْهِمْ حَافِظِينَSorah Al-Mutaffifin (Those Who Deal in Fraud) Verse Number 33
Na wao hawakutumwa wawe walinzi juu yao.
فَالْيَوْمَ الَّذِينَ آمَنُواْ مِنَ الْكُفَّارِ يَضْحَكُونَSorah Al-Mutaffifin (Those Who Deal in Fraud) Verse Number 34
Basi leo walio amini ndio watawacheka makafiri,
عَلَى الأَرَائِكِ يَنظُرُونَSorah Al-Mutaffifin (Those Who Deal in Fraud) Verse Number 35
Nao wako juu ya viti vya enzi wakiangalia.
هَلْ ثُوِّبَ الْكُفَّارُ مَا كَانُوا يَفْعَلُونَSorah Al-Mutaffifin (Those Who Deal in Fraud) Verse Number 36
Je! makafiri wamelipwa malipo ya yale waliyo kuwa wakiyatenda?