Swahili
Sorah Nooh

Verses Number 28

إِنَّا أَرْسَلْنَا نُوحًا إِلَى قَوْمِهِ أَنْ أَنذِرْ قَوْمَكَ مِن قَبْلِ أَن يَأْتِيَهُمْ عَذَابٌ أَلِيمٌSorah Nooh Verse Number 1
Hakika Sisi tulimtuma Nuh'u kwa watu wake: Uwaonye kaumu yako kabla ya kuwafikia adhabu chungu.
قَالَ يَا قَوْمِ إِنِّي لَكُمْ نَذِيرٌ مُّبِينٌSorah Nooh Verse Number 2
Akasema: Enyi watu wangu! Kwa hakika mimi ni mwonyaji wa dhaahiri kwenu,
أَنِ اعْبُدُوا اللَّهَ وَاتَّقُوهُ وَأَطِيعُونِSorah Nooh Verse Number 3
Ya kwamba mumuabudu Mwenyezi Mungu, na mumche Yeye, na mumt'ii.
يَغْفِرْ لَكُم مِّن ذُنُوبِكُمْ وَيُؤَخِّرْكُمْ إِلَى أَجَلٍ مُّسَمًّى إِنَّ أَجَلَ اللَّهِ إِذَا جَاءَ لا يُؤَخَّرُ لَوْ كُنتُمْ تَعْلَمُونَSorah Nooh Verse Number 4
Atakughufirieni madhambi yenu, na atakuakhirisheni mpaka muda ulio wekwa. Hakika muda wa Mwenyezi Mungu utapo fika haucheleweshwi. Laiti mngejua!
قَالَ رَبِّ إِنِّي دَعَوْتُ قَوْمِي لَيْلا وَنَهَارًاSorah Nooh Verse Number 5
Akasema: Ee Mola wangu Mlezi! Hakika mimi nimewaita watu wangu usiku na mchana,
فَلَمْ يَزِدْهُمْ دُعَائِي إِلاَّ فِرَارًاSorah Nooh Verse Number 6
Lakini wito wangu haukuwazidisha ila kukimbia.
وَإِنِّي كُلَّمَا دَعَوْتُهُمْ لِتَغْفِرَ لَهُمْ جَعَلُوا أَصَابِعَهُمْ فِي آذَانِهِمْ وَاسْتَغْشَوْا ثِيَابَهُمْ وَأَصَرُّوا وَاسْتَكْبَرُوا اسْتِكْبَارًاSorah Nooh Verse Number 7
Na hakika mimi kila nilipo waita ili upate kuwaghufiria, walijiziba masikio yao kwa vidole vyao, na wakajigubika nguo zao, na wakakamia, na wakatakabari vikubwa mno!
ثُمَّ إِنِّي دَعَوْتُهُمْ جِهَارًاSorah Nooh Verse Number 8
Tena niliwaita kwa uwazi,
ثُمَّ إِنِّي أَعْلَنتُ لَهُمْ وَأَسْرَرْتُ لَهُمْ إِسْرَارًاSorah Nooh Verse Number 9
Kisha nikawatangazia kwa kelele, tena nikasema nao kwa siri.
فَقُلْتُ اسْتَغْفِرُوا رَبَّكُمْ إِنَّهُ كَانَ غَفَّارًاSorah Nooh Verse Number 10
Nikasema: Ombeni msamaha kwa Mola wenu Mlezi; hakika Yeye ni Mwingi wa kusamehe.
يُرْسِلِ السَّمَاء عَلَيْكُم مِّدْرَارًاSorah Nooh Verse Number 11
Atakuleteeni mvua inyeshe mfululizo.
وَيُمْدِدْكُمْ بِأَمْوَالٍ وَبَنِينَ وَيَجْعَل لَّكُمْ جَنَّاتٍ وَيَجْعَل لَّكُمْ أَنْهَارًاSorah Nooh Verse Number 12
Na atakupeni mali na wana, na atakupeni mabustani na atakufanyieni mito.
مَّا لَكُمْ لا تَرْجُونَ لِلَّهِ وَقَارًاSorah Nooh Verse Number 13
Mna nini hamweki heshima ya Mwenyezi Mungu?
وَقَدْ خَلَقَكُمْ أَطْوَارًاSorah Nooh Verse Number 14
Na hali Yeye kakuumbeni daraja baada ya daraja?
أَلَمْ تَرَوْا كَيْفَ خَلَقَ اللَّهُ سَبْعَ سَمَاوَاتٍ طِبَاقًاSorah Nooh Verse Number 15
Kwani hamwoni jinsi Mwenyezi Mungu alivyo ziumba mbingu saba kwa matabaka?
وَجَعَلَ الْقَمَرَ فِيهِنَّ نُورًا وَجَعَلَ الشَّمْسَ سِرَاجًاSorah Nooh Verse Number 16
Na akaufanya mwezi ndani yake uwe nuru, na akalifanya jua kuwa taa?
وَاللَّهُ أَنبَتَكُم مِّنَ الأَرْضِ نَبَاتًاSorah Nooh Verse Number 17
Na Mwenyezi Mungu amekuotesheni katika ardhi kama mimea.
ثُمَّ يُعِيدُكُمْ فِيهَا وَيُخْرِجُكُمْ إِخْرَاجًاSorah Nooh Verse Number 18
Kisha atakurudsheni humo na atakutoeni tena.
وَاللَّهُ جَعَلَ لَكُمُ الأَرْضَ بِسَاطًاSorah Nooh Verse Number 19
Na Mwenyezi Mungu amekukunjulieni ardhi kama busati.
لِتَسْلُكُوا مِنْهَا سُبُلا فِجَاجًاSorah Nooh Verse Number 20
Ili mtembee humo katika njia zilizo pana.
قَالَ نُوحٌ رَّبِّ إِنَّهُمْ عَصَوْنِي وَاتَّبَعُوا مَن لَّمْ يَزِدْهُ مَالُهُ وَوَلَدُهُ إِلاَّ خَسَارًاSorah Nooh Verse Number 21
Nuh'u akasema: Mola wangu Mlezi! Hakika hao wameniasi, na wamemfuata yule ambaye mali yake na wanawe hawakumzidishia ila khasara.
وَمَكَرُوا مَكْرًا كُبَّارًاSorah Nooh Verse Number 22
Na wakapanga vitimbi vikubwa.
وَقَالُوا لا تَذَرُنَّ آلِهَتَكُمْ وَلا تَذَرُنَّ وَدًّا وَلا سُوَاعًا وَلا يَغُوثَ وَيَعُوقَ وَنَسْرًاSorah Nooh Verse Number 23
Na wakasema: Msiwaache miungu yenu, wala msimwache Wadda wala Suwaa' wala Yaghutha, wala Yau'qa, wala Nasra.
وَقَدْ أَضَلُّوا كَثِيرًا وَلا تَزِدِ الظَّالِمِينَ إِلاَّ ضَلالاSorah Nooh Verse Number 24
Na hao walikwisha wapoteza wengi, wala usiwazidishie walio dhulumu ila kupotea.
مِمَّا خَطِيئَاتِهِمْ أُغْرِقُوا فَأُدْخِلُوا نَارًا فَلَمْ يَجِدُوا لَهُم مِّن دُونِ اللَّهِ أَنصَارًاSorah Nooh Verse Number 25
Basi kwa ajili ya makosa yao waligharikishwa wakaingizwa Motoni, wala hawakuwapata wa kuwanusuru badala ya Mwenyezi Mungu.
وَقَالَ نُوحٌ رَّبِّ لا تَذَرْ عَلَى الأَرْضِ مِنَ الْكَافِرِينَ دَيَّارًاSorah Nooh Verse Number 26
Na Nuh'u akasema: Mola wangu Mlezi! Usimwache juu ya ardhi mkaazi wake yeyote katika makafiri!
إِنَّكَ إِن تَذَرْهُمْ يُضِلُّوا عِبَادَكَ وَلا يَلِدُوا إِلاَّ فَاجِرًا كَفَّارًاSorah Nooh Verse Number 27
Hakika ukiwaacha watawapoteza waja wako, wala wao hawatazaa ila waovu makafiri.
رَبِّ اغْفِرْ لِي وَلِوَالِدَيَّ وَلِمَن دَخَلَ بَيْتِيَ مُؤْمِنًا وَلِلْمُؤْمِنِينَ وَالْمُؤْمِنَاتِ وَلا تَزِدِ الظَّالِمِينَ إِلاَّ تَبَارًاSorah Nooh Verse Number 28
Mola wangu Mlezi! Nighufirie mimi na wazazi wangu, na kila aliye ingia nyumbani mwangu kuwa ni mwenye kuamini, na Waumini wote wanaume, na Waumini wanawake. Na wala usiwazidishie walio dhulumu ila kupotea.