Swahili
Sorah Al-Ma'arij (The Ways of Ascent )

Verses Number 44

سَأَلَ سَائِلٌ بِعَذَابٍ وَاقِعٍSorah Al-Ma'arij (The Ways of Ascent ) Verse Number 1
Muulizaji aliuliza juu ya adhabu itakayo tokea,
لِّلْكَافِرِينَ لَيْسَ لَهُ دَافِعٌSorah Al-Ma'arij (The Ways of Ascent ) Verse Number 2
Kwa makafiri - ambayo hapana awezaye kuizuia -
مِّنَ اللَّهِ ذِي الْمَعَارِجِSorah Al-Ma'arij (The Ways of Ascent ) Verse Number 3
Kutoka kwa Mwenyezi Mungu Mwenye mbingu za daraja.
تَعْرُجُ الْمَلائِكَةُ وَالرُّوحُ إِلَيْهِ فِي يَوْمٍ كَانَ مِقْدَارُهُ خَمْسِينَ أَلْفَ سَنَةٍSorah Al-Ma'arij (The Ways of Ascent ) Verse Number 4
Malaika na Roho hupanda kwendea kwake katika siku ambayo kadiri yake ni miaka khamsini elfu!
فَاصْبِرْ صَبْرًا جَمِيلاSorah Al-Ma'arij (The Ways of Ascent ) Verse Number 5
Basi subiri kwa subira njema.
إِنَّهُمْ يَرَوْنَهُ بَعِيدًاSorah Al-Ma'arij (The Ways of Ascent ) Verse Number 6
Hakika wao wanaiona iko mbali,
وَنَرَاهُ قَرِيبًاSorah Al-Ma'arij (The Ways of Ascent ) Verse Number 7
Na Sisi tunaiona iko karibu.
يَوْمَ تَكُونُ السَّمَاء كَالْمُهْلِSorah Al-Ma'arij (The Ways of Ascent ) Verse Number 8
Siku ambayo mbingu zitakapo kuwa kama maadeni iliyo yayushwa.
وَتَكُونُ الْجِبَالُ كَالْعِهْنِSorah Al-Ma'arij (The Ways of Ascent ) Verse Number 9
Na milima itakuwa kama sufi.
وَلا يَسْأَلُ حَمِيمٌ حَمِيمًاSorah Al-Ma'arij (The Ways of Ascent ) Verse Number 10
Wala jamaa hatamuuliza jamaa yake.
يُبَصَّرُونَهُمْ يَوَدُّ الْمُجْرِمُ لَوْ يَفْتَدِي مِنْ عَذَابِ يَوْمِئِذٍ بِبَنِيهِSorah Al-Ma'arij (The Ways of Ascent ) Verse Number 11
Ijapo kuwa wataonyeshwa waonane. Atatamani mkosefu lau ajikomboe na adhabu ya siku hiyo kwa kuwatoa fidia wanawe,
وَصَاحِبَتِهِ وَأَخِيهِSorah Al-Ma'arij (The Ways of Ascent ) Verse Number 12
Na mkewe, na nduguye,
وَفَصِيلَتِهِ الَّتِي تُؤْويهِSorah Al-Ma'arij (The Ways of Ascent ) Verse Number 13
Na jamaa zake walio kuwa wakimkimu,
وَمَن فِي الأَرْضِ جَمِيعًا ثُمَّ يُنجِيهِSorah Al-Ma'arij (The Ways of Ascent ) Verse Number 14
Na wote waliomo duniani, kisha aokoke yeye.
كَلاَّ إِنَّهَا لَظَىSorah Al-Ma'arij (The Ways of Ascent ) Verse Number 15
La, hasha! Kwa hakika huo ni Moto mkali kabisa,
نَزَّاعَةً لِّلشَّوَىSorah Al-Ma'arij (The Ways of Ascent ) Verse Number 16
Unao babua ngozi ya kichwa!
تَدْعُو مَنْ أَدْبَرَ وَتَوَلَّىSorah Al-Ma'arij (The Ways of Ascent ) Verse Number 17
Utamwita kila aliye geuza mgongo na akageuka.
وَجَمَعَ فَأَوْعَىSorah Al-Ma'arij (The Ways of Ascent ) Verse Number 18
Na akakusanya mali, kisha akayahifadhi.
إِنَّ الإِنسَانَ خُلِقَ هَلُوعًاSorah Al-Ma'arij (The Ways of Ascent ) Verse Number 19
Hakika mtu ameumbwa na papara.
إِذَا مَسَّهُ الشَّرُّ جَزُوعًاSorah Al-Ma'arij (The Ways of Ascent ) Verse Number 20
Inapo mgusa shari hupapatika.
وَإِذَا مَسَّهُ الْخَيْرُ مَنُوعًاSorah Al-Ma'arij (The Ways of Ascent ) Verse Number 21
Na inapo mgusa kheri huizuilia.
إِلاَّ الْمُصَلِّينَSorah Al-Ma'arij (The Ways of Ascent ) Verse Number 22
Isipo kuwa wanao sali,
الَّذِينَ هُمْ عَلَى صَلاتِهِمْ دَائِمُونَSorah Al-Ma'arij (The Ways of Ascent ) Verse Number 23
Ambao wanadumisha Sala zao,
وَالَّذِينَ فِي أَمْوَالِهِمْ حَقٌّ مَّعْلُومٌSorah Al-Ma'arij (The Ways of Ascent ) Verse Number 24
Na ambao katika mali yao iko haki maalumu
لِّلسَّائِلِ وَالْمَحْرُومِSorah Al-Ma'arij (The Ways of Ascent ) Verse Number 25
Kwa mwenye kuomba na anaye jizuilia kuomba;
وَالَّذِينَ يُصَدِّقُونَ بِيَوْمِ الدِّينِSorah Al-Ma'arij (The Ways of Ascent ) Verse Number 26
Na ambao wanaisadiki Siku ya Malipo,
وَالَّذِينَ هُم مِّنْ عَذَابِ رَبِّهِم مُّشْفِقُونَSorah Al-Ma'arij (The Ways of Ascent ) Verse Number 27
Na ambao wanaiogopa adhabu itokayo kwa Mola wao Mlezi.
إِنَّ عَذَابَ رَبِّهِمْ غَيْرُ مَأْمُونٍSorah Al-Ma'arij (The Ways of Ascent ) Verse Number 28
Hakika adhabu ya Mola wao Mlezi si ya kuaminika nayo.
وَالَّذِينَ هُمْ لِفُرُوجِهِمْ حَافِظُونَSorah Al-Ma'arij (The Ways of Ascent ) Verse Number 29
Na ambao wanahifadhi tupu zao.
إِلاَّ عَلَى أَزْوَاجِهِمْ أَوْ مَا مَلَكَتْ أَيْمَانُهُمْ فَإِنَّهُمْ غَيْرُ مَلُومِينَSorah Al-Ma'arij (The Ways of Ascent ) Verse Number 30
Isipo kuwa kwa wake zao, au iliyo wamiliki mikono yao ya kuume, basi hao hawalaumiwi -
فَمَنِ ابْتَغَى وَرَاء ذَلِكَ فَأُولَئِكَ هُمُ الْعَادُونَSorah Al-Ma'arij (The Ways of Ascent ) Verse Number 31
Lakini wanao taka kinyume ya haya, basi hao ndio wanao ruka mipaka.
وَالَّذِينَ هُمْ لِأَمَانَاتِهِمْ وَعَهْدِهِمْ رَاعُونَSorah Al-Ma'arij (The Ways of Ascent ) Verse Number 32
Na ambao wanazichunga amana zao na ahadi zao,
وَالَّذِينَ هُم بِشَهَادَاتِهِمْ قَائِمُونَSorah Al-Ma'arij (The Ways of Ascent ) Verse Number 33
Na ambao wanasimama imara katika ushahidi wao,
وَالَّذِينَ هُمْ عَلَى صَلاتِهِمْ يُحَافِظُونَSorah Al-Ma'arij (The Ways of Ascent ) Verse Number 34
Na ambao wanazihifadhi Sala zao.
أُوْلَئِكَ فِي جَنَّاتٍ مُّكْرَمُونَSorah Al-Ma'arij (The Ways of Ascent ) Verse Number 35
Hao ndio watakao hishimiwa Peponi.
فَمَالِ الَّذِينَ كَفَرُوا قِبَلَكَ مُهْطِعِينَSorah Al-Ma'arij (The Ways of Ascent ) Verse Number 36
Wana nini wale walio kufuru wanakutumbulia macho tu?
عَنِ الْيَمِينِ وَعَنِ الشِّمَالِ عِزِينَSorah Al-Ma'arij (The Ways of Ascent ) Verse Number 37
Makundi kwa makundi upande wa kulia na upande wa kushoto!
أَيَطْمَعُ كُلُّ امْرِئٍ مِّنْهُمْ أَن يُدْخَلَ جَنَّةَ نَعِيمٍSorah Al-Ma'arij (The Ways of Ascent ) Verse Number 38
Kwani kila mmoja wao anatumai kuingizwa katika Pepo ya neema?
كَلاَّ إِنَّا خَلَقْنَاهُم مِّمَّا يَعْلَمُونَSorah Al-Ma'arij (The Ways of Ascent ) Verse Number 39
La, hasha! Hakika Sisi tumewaumba kutokana na wanacho kijua.
فَلا أُقْسِمُ بِرَبِّ الْمَشَارِقِ وَالْمَغَارِبِ إِنَّا لَقَادِرُونَSorah Al-Ma'arij (The Ways of Ascent ) Verse Number 40
Basi naapa kwa Mola Mlezi wa mashariki zote na magharibi zote kwamba Sisi tunaweza
عَلَى أَن نُّبَدِّلَ خَيْرًا مِّنْهُمْ وَمَا نَحْنُ بِمَسْبُوقِينَSorah Al-Ma'arij (The Ways of Ascent ) Verse Number 41
Kuwabadili kwa walio bora kuliko wao; na Sisi hatushindwi.
فَذَرْهُمْ يَخُوضُوا وَيَلْعَبُوا حَتَّى يُلاقُوا يَوْمَهُمُ الَّذِي يُوعَدُونَSorah Al-Ma'arij (The Ways of Ascent ) Verse Number 42
Basi waache wapige porojo na wacheze, mpaka wakutane na siku yao wanayo ahidiwa,
يَوْمَ يَخْرُجُونَ مِنَ الأَجْدَاثِ سِرَاعًا كَأَنَّهُمْ إِلَى نُصُبٍ يُوفِضُونَSorah Al-Ma'arij (The Ways of Ascent ) Verse Number 43
Siku watakapotoka makaburini kwa upesi kama kwamba wanakimbilia mfundo,
خَاشِعَةً أَبْصَارُهُمْ تَرْهَقُهُمْ ذِلَّةٌ ذَلِكَ الْيَوْمُ الَّذِي كَانُوا يُوعَدُونَSorah Al-Ma'arij (The Ways of Ascent ) Verse Number 44
Macho yao yatainama, fedheha itawafunika. Hiyo ndiyo Siku waliyo kuwa wakiahidiwa.