Swahili
Sorah Qaf ( The Letter Qaf )

Verses Number 45

ق وَالْقُرْآنِ الْمَجِيدِSorah Qaf ( The Letter Qaf ) Verse Number 1
Qaaf. Naapa kwa Qur'ani tukufu!
بَلْ عَجِبُوا أَن جَاءَهُمْ مُنذِرٌ مِّنْهُمْ فَقَالَ الْكَافِرُونَ هَذَا شَيْءٌ عَجِيبٌSorah Qaf ( The Letter Qaf ) Verse Number 2
Bali wanastaajabu kwamba amewafikia mwonyaji kutoka miongoni mwao, na wakasema makafiri: Hili ni jambo la ajabu!
أَءِذَا مِتْنَا وَكُنَّا تُرَابًا ذَلِكَ رَجْعٌ بَعِيدٌSorah Qaf ( The Letter Qaf ) Verse Number 3
Ati tukifa na tukawa udongo...? Kurejea huko kuko mbali!
قَدْ عَلِمْنَا مَا تَنقُصُ الأَرْضُ مِنْهُمْ وَعِندَنَا كِتَابٌ حَفِيظٌSorah Qaf ( The Letter Qaf ) Verse Number 4
Hakika Sisi tunajua kiasi cha kila kinacho punguzwa na ardhi kutokana nao. Na kwetu kipo Kitabu kinacho hifadhi yote.
بَلْ كَذَّبُوا بِالْحَقِّ لَمَّا جَاءَهُمْ فَهُمْ فِي أَمْرٍ مَّرِيجٍSorah Qaf ( The Letter Qaf ) Verse Number 5
Lakini waliikanusha Haki ilipo wajia; kwa hivyo wamo katika mambo ya mkorogo.
أَفَلَمْ يَنظُرُوا إِلَى السَّمَاء فَوْقَهُمْ كَيْفَ بَنَيْنَاهَا وَزَيَّنَّاهَا وَمَا لَهَا مِن فُرُوجٍSorah Qaf ( The Letter Qaf ) Verse Number 6
Je! Hawaangalii mbingu zilizo juu yao! Vipi tulivyo zijenga, na tukazipamba. Wala hazina nyufa.
وَالأَرْضَ مَدَدْنَاهَا وَأَلْقَيْنَا فِيهَا رَوَاسِيَ وَأَنبَتْنَا فِيهَا مِن كُلِّ زَوْجٍ بَهِيجٍSorah Qaf ( The Letter Qaf ) Verse Number 7
Na ardhi tumeitandaza na tukaiwekea milima, na tukaiotesha mimea mizuri ya kila namna.
تَبْصِرَةً وَذِكْرَى لِكُلِّ عَبْدٍ مُّنِيبٍSorah Qaf ( The Letter Qaf ) Verse Number 8
Yawe haya ni kifumbua macho na ukumbusho kwa kila mja mwenye kuelekea.
وَنَزَّلْنَا مِنَ السَّمَاءِ مَاءً مُّبَارَكًا فَأَنبَتْنَا بِهِ جَنَّاتٍ وَحَبَّ الْحَصِيدِSorah Qaf ( The Letter Qaf ) Verse Number 9
Na tumeteremsha kutoka mbinguni maji yaliyo barikiwa, na kwa hayo tukaotesha mabustani na nafaka za kuvunwa.
وَالنَّخْلَ بَاسِقَاتٍ لَّهَا طَلْعٌ نَّضِيدٌSorah Qaf ( The Letter Qaf ) Verse Number 10
Na mitende mirefu yenye makole yaliyo zaa kwa wingi,
رِزْقًا لِّلْعِبَادِ وَأَحْيَيْنَا بِهِ بَلْدَةً مَّيْتًا كَذَلِكَ الْخُرُوجُSorah Qaf ( The Letter Qaf ) Verse Number 11
Ili iwe ni riziki kwa waja wangu. Na tukaifufua kwa maji nchi iliyo kuwa imekufa. Kama hivyo ndivyo utakavyo kuwa ufufuaji.
كَذَّبَتْ قَبْلَهُمْ قَوْمُ نُوحٍ وَأَصْحَابُ الرَّسِّ وَثَمُودُSorah Qaf ( The Letter Qaf ) Verse Number 12
Kabla yao walikadhibisha kaumu ya Nuhu na wakaazi wa Rassi na Thamudi.
وَعَادٌ وَفِرْعَوْنُ وَإِخْوَانُ لُوطٍSorah Qaf ( The Letter Qaf ) Verse Number 13
Na A'di na Firauni na kaumu ya Lut'i.
وَأَصْحَابُ الأَيْكَةِ وَقَوْمُ تُبَّعٍ كُلٌّ كَذَّبَ الرُّسُلَ فَحَقَّ وَعِيدِSorah Qaf ( The Letter Qaf ) Verse Number 14
Na wakaazi wa Machakani, na watu wa Tubbaa'. Wote hao waliwakanusha Mitume, kwa hivyo onyo likathibitika juu yao.
أَفَعَيِينَا بِالْخَلْقِ الأَوَّلِ بَلْ هُمْ فِي لَبْسٍ مِّنْ خَلْقٍ جَدِيدٍSorah Qaf ( The Letter Qaf ) Verse Number 15
Kwani tulichoka kwa kuumba mara ya kwanza. Bali wao wamo katika shaka tu juu ya umbo jipya.
وَلَقَدْ خَلَقْنَا الإِنسَانَ وَنَعْلَمُ مَا تُوَسْوِسُ بِهِ نَفْسُهُ وَنَحْنُ أَقْرَبُ إِلَيْهِ مِنْ حَبْلِ الْوَرِيدِSorah Qaf ( The Letter Qaf ) Verse Number 16
Na hakika tumemuumba mtu, nasi tunayajua yanayo mpitikia katika nafsi yake. Na Sisi tuko karibu naye kuliko mshipa wa shingoni mwake.
إِذْ يَتَلَقَّى الْمُتَلَقِّيَانِ عَنِ الْيَمِينِ وَعَنِ الشِّمَالِ قَعِيدٌSorah Qaf ( The Letter Qaf ) Verse Number 17
Wanapo pokea wapokeaji wawili, wanao kaa kuliani na kushotoni.
مَا يَلْفِظُ مِن قَوْلٍ إِلاَّ لَدَيْهِ رَقِيبٌ عَتِيدٌSorah Qaf ( The Letter Qaf ) Verse Number 18
Hatamki neno ila karibu yake yupo mwangalizi tayari.
وَجَاءَتْ سَكْرَةُ الْمَوْتِ بِالْحَقِّ ذَلِكَ مَا كُنتَ مِنْهُ تَحِيدُSorah Qaf ( The Letter Qaf ) Verse Number 19
Na uchungu wa kutoka roho utamjia kwa haki. Hayo ndiyo uliyo kuwa ukiyakimbia.
وَنُفِخَ فِي الصُّورِ ذَلِكَ يَوْمُ الْوَعِيدِSorah Qaf ( The Letter Qaf ) Verse Number 20
Na litapulizwa baragumu. Hiyo ndiyo Siku ya Miadi.
وَجَاءَتْ كُلُّ نَفْسٍ مَّعَهَا سَائِقٌ وَشَهِيدٌSorah Qaf ( The Letter Qaf ) Verse Number 21
Na kila nafsi itakuja na pamoja nayo mchungaji na shahidi.
لَقَدْ كُنتَ فِي غَفْلَةٍ مِّنْ هَذَا فَكَشَفْنَا عَنكَ غِطَاءَكَ فَبَصَرُكَ الْيَوْمَ حَدِيدٌSorah Qaf ( The Letter Qaf ) Verse Number 22
(Aambiwe): Kwa hakika ulikuwa umeghafilika na haya; basi leo tumekuondolea pazia lako, na kwa hivyo kuona kwako leo ni kukali.
وَقَالَ قَرِينُهُ هَذَا مَا لَدَيَّ عَتِيدٌSorah Qaf ( The Letter Qaf ) Verse Number 23
Na mwenzake atasema: Huyu niliye naye mimi kesha tayarishwa.
أَلْقِيَا فِي جَهَنَّمَ كُلَّ كَفَّارٍ عَنِيدٍSorah Qaf ( The Letter Qaf ) Verse Number 24
Mtupeni katika Jahannamu kila kafiri mwenye inda,
مَّنَّاعٍ لِّلْخَيْرِ مُعْتَدٍ مُّرِيبٍSorah Qaf ( The Letter Qaf ) Verse Number 25
Akatazaye kheri, arukaye mipaka, mwenye kutia shaka,
الَّذِي جَعَلَ مَعَ اللَّهِ إِلَهًا آخَرَ فَأَلْقِيَاهُ فِي الْعَذَابِ الشَّدِيدِSorah Qaf ( The Letter Qaf ) Verse Number 26
Aliye weka mungu mwengine pamoja na Mwenyezi Mungu. Basi mtupeni katika adhabu kali.
قَالَ قَرِينُهُ رَبَّنَا مَا أَطْغَيْتُهُ وَلَكِن كَانَ فِي ضَلالٍ بَعِيدٍSorah Qaf ( The Letter Qaf ) Verse Number 27
Mwenzake aseme: Ee Mola wetu Mlezi! Sikumpoteza mimi, bali yeye mwenyewe alikuwa katika upotovu wa mbali.
قَالَ لا تَخْتَصِمُوا لَدَيَّ وَقَدْ قَدَّمْتُ إِلَيْكُم بِالْوَعِيدِSorah Qaf ( The Letter Qaf ) Verse Number 28
(Mwenyezi Mungu) aseme: Msigombane mbele yangu. Nilikuleteeni mbele onyo langu.
مَا يُبَدَّلُ الْقَوْلُ لَدَيَّ وَمَا أَنَا بِظَلاَّمٍ لِّلْعَبِيدِSorah Qaf ( The Letter Qaf ) Verse Number 29
Mbele yangu haibadilishwi kauli, wala Mimi siwadhulumu waja wangu.
يَوْمَ نَقُولُ لِجَهَنَّمَ هَلِ امْتَلَأْتِ وَتَقُولُ هَلْ مِن مَّزِيدٍSorah Qaf ( The Letter Qaf ) Verse Number 30
Siku tutapo iambia Jahannamu: Je! Umejaa? Nayo itasema: Je! Kuna ziada?
وَأُزْلِفَتِ الْجَنَّةُ لِلْمُتَّقِينَ غَيْرَ بَعِيدٍSorah Qaf ( The Letter Qaf ) Verse Number 31
Na Pepo italetwa karibu kwa ajili ya wachamngu, haitakuwa mbali.
هَذَا مَا تُوعَدُونَ لِكُلِّ أَوَّابٍ حَفِيظٍSorah Qaf ( The Letter Qaf ) Verse Number 32
Haya ndiyo mnayo ahidiwa kwa kila mwenye kurejea kwa Mwenyezi Mungu na akajilinda.
مَنْ خَشِيَ الرَّحْمَن بِالْغَيْبِ وَجَاءَ بِقَلْبٍ مُّنِيبٍSorah Qaf ( The Letter Qaf ) Verse Number 33
Mwenye kumwogopa Mwingi wa Rehema hali kuwa hamwoni, na akaja kwa moyo ulio elekea-
ادْخُلُوهَا بِسَلامٍ ذَلِكَ يَوْمُ الْخُلُودِSorah Qaf ( The Letter Qaf ) Verse Number 34
(Ataambiwa) ingieni kwa salama. Hiyo ndiyo siku ya daima dawamu.
لَهُم مَّا يَشَاؤُونَ فِيهَا وَلَدَيْنَا مَزِيدٌSorah Qaf ( The Letter Qaf ) Verse Number 35
Humo watapata wakitakacho, na kwetu yako ya ziada.
وَكَمْ أَهْلَكْنَا قَبْلَهُم مِّن قَرْنٍ هُمْ أَشَدُّ مِنْهُم بَطْشًا فَنَقَّبُوا فِي الْبِلادِ هَلْ مِن مَّحِيصٍSorah Qaf ( The Letter Qaf ) Verse Number 36
Na kaumu ngapi tuliziangamiza kabla yao walio kuwa na nguvu zaidi kuliko hawa! Nao walitanga tanga katika nchi nyingi. Je! Walipata pa kukimbilia?
إِنَّ فِي ذَلِكَ لَذِكْرَى لِمَن كَانَ لَهُ قَلْبٌ أَوْ أَلْقَى السَّمْعَ وَهُوَ شَهِيدٌSorah Qaf ( The Letter Qaf ) Verse Number 37
Hakika katika hayo upo ukumbusho kwa mwenye moyo au akatega sikio naye yupo anashuhudia.
وَلَقَدْ خَلَقْنَا السَّمَاوَاتِ وَالأَرْضَ وَمَا بَيْنَهُمَا فِي سِتَّةِ أَيَّامٍ وَمَا مَسَّنَا مِن لُّغُوبٍSorah Qaf ( The Letter Qaf ) Verse Number 38
Na bila ya shaka Sisi tumeziumba mbingu na ardhi na vilio baina yao mnamo siku sita; na wala hayakutugusa machofu.
فَاصْبِرْ عَلَى مَا يَقُولُونَ وَسَبِّحْ بِحَمْدِ رَبِّكَ قَبْلَ طُلُوعِ الشَّمْسِ وَقَبْلَ الْغُرُوبِSorah Qaf ( The Letter Qaf ) Verse Number 39
Basi vumilia kwa hayo wasemayo, na mtakase kwa kumsifu Mola wako Mlezi kabla ya kuchomoza jua na kabla ya kuchwa.
وَمِنَ اللَّيْلِ فَسَبِّحْهُ وَأَدْبَارَ السُّجُودِSorah Qaf ( The Letter Qaf ) Verse Number 40
Na katika usiku pia mtakase, na baada ya kusujudu.
وَاسْتَمِعْ يَوْمَ يُنَادِ الْمُنَادِ مِن مَّكَانٍ قَرِيبٍSorah Qaf ( The Letter Qaf ) Verse Number 41
Na sikiliza siku atapo nadi mwenye kunadi kutoka pahala karibu.
يَوْمَ يَسْمَعُونَ الصَّيْحَةَ بِالْحَقِّ ذَلِكَ يَوْمُ الْخُرُوجِSorah Qaf ( The Letter Qaf ) Verse Number 42
Siku watakapo sikia ukelele wa haki. Hiyo ndiyo siku ya kufufuka.
إِنَّا نَحْنُ نُحْيِي وَنُمِيتُ وَإِلَيْنَا الْمَصِيرُSorah Qaf ( The Letter Qaf ) Verse Number 43
Hakika Sisi tunahuisha na tunafisha, na kwetu Sisi ndio marejeo.
يَوْمَ تَشَقَّقُ الأَرْضُ عَنْهُمْ سِرَاعًا ذَلِكَ حَشْرٌ عَلَيْنَا يَسِيرٌSorah Qaf ( The Letter Qaf ) Verse Number 44
Siku itapo wapasukia ardhi mbio mbio! Mkusanyo huo kwetu ni mwepesi.
نَحْنُ أَعْلَمُ بِمَا يَقُولُونَ وَمَا أَنتَ عَلَيْهِم بِجَبَّارٍ فَذَكِّرْ بِالْقُرْآنِ مَن يَخَافُ وَعِيدِSorah Qaf ( The Letter Qaf ) Verse Number 45
Sisi tunajua kabisa wayasemayo. Wala wewe si mwenye kuwatawalia kwa ujabari. Basi mkumbushe kwa Qur'ani anaye liogopa onyo.