Swahili
Sorah Sad ( The Letter Sad )

Verses Number 88

ص وَالْقُرْآنِ ذِي الذِّكْرِSorah Sad ( The Letter Sad ) Verse Number 1
S'ad, Naapa kwa Qur'ani yenye mawaidha.
بَلِ الَّذِينَ كَفَرُوا فِي عِزَّةٍ وَشِقَاقٍSorah Sad ( The Letter Sad ) Verse Number 2
Lakini walio kufuru wamo katika majivuno na upinzani
كَمْ أَهْلَكْنَا مِن قَبْلِهِم مِّن قَرْنٍ فَنَادَوْا وَلاتَ حِينَ مَنَاصٍSorah Sad ( The Letter Sad ) Verse Number 3
Mataifa mangapi tumeyaangamiza kabla yao, na wakapiga kelele, lakini wakati wa kuokoka ulikwisha pita.
وَعَجِبُوا أَن جَاءَهُم مُّنذِرٌ مِّنْهُمْ وَقَالَ الْكَافِرُونَ هَذَا سَاحِرٌ كَذَّابٌSorah Sad ( The Letter Sad ) Verse Number 4
Na walistaajabu kuwajia mwonyaji anaye tokana nao wenyewe, na makafiri wakasema: Huyu ni mchawi, mwongo.
أَجَعَلَ الآلِهَةَ إِلَهًا وَاحِدًا إِنَّ هَذَا لَشَيْءٌ عُجَابٌSorah Sad ( The Letter Sad ) Verse Number 5
Amewafanya miungu wote kuwa ni Mungu Mmoja tu? Hakika hili ni jambo la ajabu.
وَانطَلَقَ الْمَلَأُ مِنْهُمْ أَنِ امْشُوا وَاصْبِرُوا عَلَى آلِهَتِكُمْ إِنَّ هَذَا لَشَيْءٌ يُرَادُSorah Sad ( The Letter Sad ) Verse Number 6
Na wakaondoka wakubwa wao wakiwaambia: Nendeni zenu na dumuni na miungu yenu, kwani hili ni jambo lililo pangwa.
مَا سَمِعْنَا بِهَذَا فِي الْمِلَّةِ الآخِرَةِ إِنْ هَذَا إِلاَّ اخْتِلاقٌSorah Sad ( The Letter Sad ) Verse Number 7
Sisi hatukusikia haya katika mila hii ya mwisho. Haya si chochote ila ni uzushi tu.
أَأُنزِلَ عَلَيْهِ الذِّكْرُ مِن بَيْنِنَا بَلْ هُمْ فِي شَكٍّ مِّن ذِكْرِي بَلْ لَمَّا يَذُوقُوا عَذَابِSorah Sad ( The Letter Sad ) Verse Number 8
Ati yeye tu ndiye aliye teremshiwa mawaidha peke yake katika sisi? Lakini hao wana shaka na mawaidha yangu, bali hawajaionja adhabu yangu.
أَمْ عِندَهُمْ خَزَائِنُ رَحْمَةِ رَبِّكَ الْعَزِيزِ الْوَهَّابِSorah Sad ( The Letter Sad ) Verse Number 9
Au wanazo wao khazina za rehema za Mola wako Mlezi, Mwenye nguvu, Mpaji?
أَمْ لَهُم مُّلْكُ السَّمَاوَاتِ وَالأَرْضِ وَمَا بَيْنَهُمَا فَلْيَرْتَقُوا فِي الأَسْبَابِSorah Sad ( The Letter Sad ) Verse Number 10
Au wao wana ufalme wa mbingu na ardhi na viliomo kati yao? Basi nawazipande njia za kwendea huko!
جُندٌ مَّا هُنَالِكَ مَهْزُومٌ مِّنَ الأَحْزَابِSorah Sad ( The Letter Sad ) Verse Number 11
Hao ni askari watao shindwa miongoni mwa makundi yatayo shindwa.
كَذَّبَتْ قَبْلَهُمْ قَوْمُ نُوحٍ وَعَادٌ وَفِرْعَوْنُ ذُو الأَوْتَادِSorah Sad ( The Letter Sad ) Verse Number 12
Walikanusha kabla yao kaumu ya Nuhu, na kina A'adi na Firauni mwenye majengo.
وَثَمُودُ وَقَوْمُ لُوطٍ وَأَصْحَابُ الأَيْكَةِ أُوْلَئِكَ الأَحْزَابُSorah Sad ( The Letter Sad ) Verse Number 13
Na Thamud na kaumu Lut'i na watu wa Machakani. Hayo ndiyo makundi.
إِن كُلٌّ إِلاَّ كَذَّبَ الرُّسُلَ فَحَقَّ عِقَابِSorah Sad ( The Letter Sad ) Verse Number 14
Hao wote waliwakadhibisha Mitume; basi wakastahiki adhabu yangu.
وَمَا يَنظُرُ هَـٰؤُلاَءِ إِلاَّ صَيْحَةً وَاحِدَةً مَّا لَهَا مِن فَوَاقٍSorah Sad ( The Letter Sad ) Verse Number 15
Na hawa hawangojei ila ukelele mmoja tu usio na muda.
وَقَالُوا رَبَّنَا عَجِّل لَّنَا قِطَّنَا قَبْلَ يَوْمِ الْحِسَابِSorah Sad ( The Letter Sad ) Verse Number 16
Na wao husema: Mola wetu Mlezi! Tuletee upesi sehemu yetu ya adhabu kabla ya Siku ya Hisabu.
اصْبِرْ عَلَى مَا يَقُولُونَ وَاذْكُرْ عَبْدَنَا دَاوُودَ ذَا الأَيْدِ إِنَّهُ أَوَّابٌSorah Sad ( The Letter Sad ) Verse Number 17
Subiri kwa hayo wayasemayo, na umkumbuke mja wetu Daudi, mwenye nguvu. Hakika yeye alikuwa mwingi wa kutubia.
إِنَّا سَخَّرْنَا الْجِبَالَ مَعَهُ يُسَبِّحْنَ بِالْعَشِيِّ وَالإِشْرَاقِSorah Sad ( The Letter Sad ) Verse Number 18
Hakika tuliidhalilisha milima pamoja naye ikisabihi jioni na asubuhi pamoja naye.
وَالطَّيْرَ مَحْشُورَةً كُلٌّ لَّهُ أَوَّابٌSorah Sad ( The Letter Sad ) Verse Number 19
Na pia ndege walio kusanywa makundi kwa makundi; wote walikuwa wanyenyekevu kwake.
وَشَدَدْنَا مُلْكَهُ وَآتَيْنَاهُ الْحِكْمَةَ وَفَصْلَ الْخِطَابِSorah Sad ( The Letter Sad ) Verse Number 20
Na tukautia nguvu ufalme wake, na tukampa hikima, na kukata hukumu.
وَهَلْ أَتَاكَ نَبَأُ الْخَصْمِ إِذْ تَسَوَّرُوا الْمِحْرَابَSorah Sad ( The Letter Sad ) Verse Number 21
Na je! Imekufikia khabari ya wagombanao walipo pindukia ukuta kuingia chumbani?
إِذْ دَخَلُوا عَلَى دَاوُودَ فَفَزِعَ مِنْهُمْ قَالُوا لا تَخَفْ خَصْمَانِ بَغَى بَعْضُنَا عَلَى بَعْضٍ فَاحْكُم بَيْنَنَا بِالْحَقِّ وَلا تُشْطِطْ وَاهْدِنَا إِلَى سَوَاءِ الصِّرَاطِSorah Sad ( The Letter Sad ) Verse Number 22
Walipo muingilia Daudi, naye akawaogopa. Wakasema: Usiogope! Sisi ni wagombanao wawili, mmoja wetu amemdhulumu mwenziwe. Basi tuhukumu kwa haki, wala usipendelee. Na utuongoe kwenye njia iliyo sawa.
إِنَّ هَذَا أَخِي لَهُ تِسْعٌ وَتِسْعُونَ نَعْجَةً وَلِيَ نَعْجَةٌ وَاحِدَةٌ فَقَالَ أَكْفِلْنِيهَا وَعَزَّنِي فِي الْخِطَابِSorah Sad ( The Letter Sad ) Verse Number 23
Hakika huyu ndugu yangu ana kondoo wa kike tisiini na tisa; na mimi ninaye kondoo mke mmoja. Akasema: Nipe huyo nikufugie! Na amenishinda kwa maneno.
قَالَ لَقَدْ ظَلَمَكَ بِسُؤَالِ نَعْجَتِكَ إِلَى نِعَاجِهِ وَإِنَّ كَثِيرًا مِّنْ الْخُلَطَاء لَيَبْغِي بَعْضُهُمْ عَلَى بَعْضٍ إِلاَّ الَّذِينَ آمَنُوا وَعَمِلُوا الصَّالِحَاتِ وَقَلِيلٌ مَّا هُمْ وَظَنَّ دَاوُودُ أَنَّمَا فَتَنَّاهُ فَاسْتَغْفَرَ رَبَّهُ وَخَرَّ رَاكِعًا وَأَنَابَSorah Sad ( The Letter Sad ) Verse Number 24
Akasema: Kweli amekudhulumu kwa kumtaka kondoo wako mmoja kuongezea kwenye kondoo wake. Na hakika washirika wengi hudhulumiana wao kwa wao, isipo kuwa walio amini na wakatenda mema. Na hao ni wachache. Na Daudi akajua kuwa tumemfanyia mtihani. Basi akamwomba msamaha Mola wake Mlezi, na akaanguka kusujudu na kutubia.
فَغَفَرْنَا لَهُ ذَلِكَ وَإِنَّ لَهُ عِندَنَا لَزُلْفَى وَحُسْنَ مَآبٍSorah Sad ( The Letter Sad ) Verse Number 25
Basi tukamsamehe kwa hayo. Naye kwa hakika anao mkaribisho mkubwa na marejeo mazuri kwetu.
يَا دَاوُودُ إِنَّا جَعَلْنَاكَ خَلِيفَةً فِي الأَرْضِ فَاحْكُم بَيْنَ النَّاسِ بِالْحَقِّ وَلا تَتَّبِعِ الْهَوَى فَيُضِلَّكَ عَن سَبِيلِ اللَّهِ إِنَّ الَّذِينَ يَضِلُّونَ عَن سَبِيلِ اللَّهِ لَهُمْ عَذَابٌ شَدِيدٌ بِمَا نَسُوا يَوْمَ الْحِسَابِSorah Sad ( The Letter Sad ) Verse Number 26
Ewe Daudi! Hakika Sisi tumekufanya wewe uwe Khalifa katika nchi. Basi wahukumu watu kwa haki, wala usifuate matamanio yakakupoteza kwenye Njia ya Mwenyezi Mungu. Hakika wanao ipotea Njia ya Mwenyezi Mungu wakaiacha, watapata adhabu kali kwa sababu ya kusahau kwao Siku ya Hisabu.
وَمَا خَلَقْنَا السَّمَاءَ وَالأَرْضَ وَمَا بَيْنَهُمَا بَاطِلاً ذَلِكَ ظَنُّ الَّذِينَ كَفَرُوا فَوَيْلٌ لِّلَّذِينَ كَفَرُوا مِنَ النَّارِSorah Sad ( The Letter Sad ) Verse Number 27
Na hatukuziumba mbingu na ardhi na viliomo ndani yao bure. Hiyo ni dhana ya walio kufuru. Ole wao walio kufuru kwa Moto utao wapata.
أَمْ نَجْعَلُ الَّذِينَ آمَنُوا وَعَمِلُوا الصَّالِحَاتِ كَالْمُفْسِدِينَ فِي الأَرْضِ أَمْ نَجْعَلُ الْمُتَّقِينَ كَالْفُجَّارِSorah Sad ( The Letter Sad ) Verse Number 28
Je! Tuwafanye walio amini na wakatenda mema kama wafanyao uharibifu katika nchi? Au tuwafanye wachamngu kama waovu?
كِتَابٌ أَنزَلْنَاهُ إِلَيْكَ مُبَارَكٌ لِّيَدَّبَّرُوا آيَاتِهِ وَلِيَتَذَكَّرَ أُوْلُوا الأَلْبَابِSorah Sad ( The Letter Sad ) Verse Number 29
Na hiki Kitabu, tumekuteremshia wewe, kimebarikiwa, ili wazizingatie Aya zake, na wawaidhike wenye akili.
وَوَهَبْنَا لِدَاوُودَ سُلَيْمَانَ نِعْمَ الْعَبْدُ إِنَّهُ أَوَّابٌSorah Sad ( The Letter Sad ) Verse Number 30
Na Daudi tukamtunukia Suleiman. Alikuwa mja mwema. Na hakika alikuwa mwingi wa kutubia.
إِذْ عُرِضَ عَلَيْهِ بِالْعَشِيِّ الصَّافِنَاتُ الْجِيَادُSorah Sad ( The Letter Sad ) Verse Number 31
Alipo pelekewa jioni farasi wasimamao kidete, tayari kutoka shoti;
فَقَالَ إِنِّي أَحْبَبْتُ حُبَّ الْخَيْرِ عَن ذِكْرِ رَبِّي حَتَّى تَوَارَتْ بِالْحِجَابِSorah Sad ( The Letter Sad ) Verse Number 32
Basi akasema: Navipenda vitu vizuri kwa kumkumbuka Mola wangu Mlezi. Kisha wakafichikana nyuma ya boma.
رُدُّوهَا عَلَيَّ فَطَفِقَ مَسْحًا بِالسُّوقِ وَالأَعْنَاقِSorah Sad ( The Letter Sad ) Verse Number 33
(Akasema:) Nirudishieni! Akaanza kuwapapasa miguu na shingo.
وَلَقَدْ فَتَنَّا سُلَيْمَانَ وَأَلْقَيْنَا عَلَى كُرْسِيِّهِ جَسَدًا ثُمَّ أَنَابَSorah Sad ( The Letter Sad ) Verse Number 34
Na tulimtia mtihanini Suleiman, na tukauweka mwili juu ya kiti chake, kisha akarejea kwa kutubu.
قَالَ رَبِّ اغْفِرْ لِي وَهَبْ لِي مُلْكًا لّا يَنبَغِي لِأَحَدٍ مِّنْ بَعْدِي إِنَّكَ أَنتَ الْوَهَّابُSorah Sad ( The Letter Sad ) Verse Number 35
Akasema: Mola wangu Mlezi! Nisamehe na unipe ufalme usio mwelekea yeyote baada yangu. Hakika Wewe ndiye Mpaji.
فَسَخَّرْنَا لَهُ الرِّيحَ تَجْرِي بِأَمْرِهِ رُخَاءً حَيْثُ أَصَابَSorah Sad ( The Letter Sad ) Verse Number 36
Basi tukaufanya upepo umtumikie, ukenda kwa amri yake, popote alipo taka kufika.
وَالشَّيَاطِينَ كُلَّ بَنَّاءٍ وَغَوَّاصٍSorah Sad ( The Letter Sad ) Verse Number 37
Na tukayafanya mashet'ani yamtumikie, wote wajenzi na wapiga mbizi.
وَآخَرِينَ مُقَرَّنِينَ فِي الأَصْفَادِSorah Sad ( The Letter Sad ) Verse Number 38
Na wengine wafungwao kwa minyororo.
هَذَا عَطَاؤُنَا فَامْنُنْ أَوْ أَمْسِكْ بِغَيْرِ حِسَابٍSorah Sad ( The Letter Sad ) Verse Number 39
Hichi ndicho kipawa chetu. Basi toa au zuia, bila ya hisabu.
وَإِنَّ لَهُ عِندَنَا لَزُلْفَى وَحُسْنَ مَآبٍSorah Sad ( The Letter Sad ) Verse Number 40
Na hakika yeye kwetu Sisi ana cheo cha kukaribishwa kwetu, na pahala pazuri pa kurejea.
وَاذْكُرْ عَبْدَنَا أَيُّوبَ إِذْ نَادَى رَبَّهُ أَنِّي مَسَّنِيَ الشَّيْطَانُ بِنُصْبٍ وَعَذَابٍSorah Sad ( The Letter Sad ) Verse Number 41
Na mkumbuke mja wetu Ayubu alipo mwita Mola wake Mlezi akasema: Kwa hakika Shet'ani amenifikishia udhia na adhabu.
ارْكُضْ بِرِجْلِكَ هَذَا مُغْتَسَلٌ بَارِدٌ وَشَرَابٌSorah Sad ( The Letter Sad ) Verse Number 42
(Akaambiwa:) Piga-piga ardhi kwa mguu wako! Basi haya maji baridi ya kuogea na ya kunywa.
وَوَهَبْنَا لَهُ أَهْلَهُ وَمِثْلَهُم مَّعَهُمْ رَحْمَةً مِّنَّا وَذِكْرَى لِأُولِي الأَلْبَابِSorah Sad ( The Letter Sad ) Verse Number 43
Na tukampa ahali zake na wengine kama wao pamoja nao, kuwa ni rehema itokayo kwetu, na iwe kumbusho kwa watu wenye akili.
وَخُذْ بِيَدِكَ ضِغْثًا فَاضْرِب بِّهِ وَلا تَحْنَثْ إِنَّا وَجَدْنَاهُ صَابِرًا نِعْمَ الْعَبْدُ إِنَّهُ أَوَّابٌSorah Sad ( The Letter Sad ) Verse Number 44
Na shika kicha cha vijiti tu mkononi mwako, kisha ndio upigie nacho, wala usivunje kiapo. Hakika tulimkuta mwenye subira, mbora wa waja, kwa hakika alikuwa mwingi wa kutubu.
وَاذْكُرْ عِبَادَنَا إِبْرَاهِيمَ وَإِسْحَاقَ وَيَعْقُوبَ أُولِي الأَيْدِي وَالأَبْصَارِSorah Sad ( The Letter Sad ) Verse Number 45
Na wakumbuke waja wetu, Ibrahim na Is-haqa na Yaa'qubu walio kuwa na nguvu na busara.
إِنَّا أَخْلَصْنَاهُم بِخَالِصَةٍ ذِكْرَى الدَّارِSorah Sad ( The Letter Sad ) Verse Number 46
Sisi tumewakhusisha wao kwa sifa ya ukumbusho wa Akhera.
وَإِنَّهُمْ عِندَنَا لَمِنَ الْمُصْطَفَيْنَ الأَخْيَارِSorah Sad ( The Letter Sad ) Verse Number 47
Na hakika wao kwetu sisi ni wateuliwa walio bora.
وَاذْكُرْ إِسْمَاعِيلَ وَالْيَسَعَ وَذَا الْكِفْلِ وَكُلٌّ مِّنْ الأَخْيَارِSorah Sad ( The Letter Sad ) Verse Number 48
Na mkumbuke Ismail na Alyasaa na Dhulkifli, na wote hao ni katika walio bora.
هَذَا ذِكْرٌ وَإِنَّ لِلْمُتَّقِينَ لَحُسْنَ مَآبٍSorah Sad ( The Letter Sad ) Verse Number 49
Huu ni ukumbusho. Na hakika wachamngu wana marudio mazuri.
جَنَّاتِ عَدْنٍ مُّفَتَّحَةً لَّهُمُ الأَبْوَابُSorah Sad ( The Letter Sad ) Verse Number 50
Bustani za milele zitazo funguliwa milango yao kwa ajili yao.
مُتَّكِئِينَ فِيهَا يَدْعُونَ فِيهَا بِفَاكِهَةٍ كَثِيرَةٍ وَشَرَابٍSorah Sad ( The Letter Sad ) Verse Number 51
Humo wataegemea matakia, wawe wanaagiza humo matunda mengi na vinywaji.
وَعِندَهُمْ قَاصِرَاتُ الطَّرْفِ أَتْرَابٌSorah Sad ( The Letter Sad ) Verse Number 52
Na pamoja nao wake zao wenye kutuliza macho, hirimu zao.
هَذَا مَا تُوعَدُونَ لِيَوْمِ الْحِسَابِSorah Sad ( The Letter Sad ) Verse Number 53
Haya ndiyo mliyo ahidiwa kwa Siku ya Hisabu.
إِنَّ هَذَا لَرِزْقُنَا مَا لَهُ مِن نَّفَادٍSorah Sad ( The Letter Sad ) Verse Number 54
Hakika hii ndiyo riziki yetu isiyo malizika.
هَذَا وَإِنَّ لِلطَّاغِينَ لَشَرَّ مَآبٍSorah Sad ( The Letter Sad ) Verse Number 55
Ndio hivi! Na hakika wenye kuasi bila ya shaka watapata marudio maovu kabisa;
جَهَنَّمَ يَصْلَوْنَهَا فَبِئْسَ الْمِهَادُSorah Sad ( The Letter Sad ) Verse Number 56
Nayo ni Jahannamu! Wataingia humo. Nacho hicho ni kitanda kiovu mno cha kulalia.
هَذَا فَلْيَذُوقُوهُ حَمِيمٌ وَغَسَّاقٌSorah Sad ( The Letter Sad ) Verse Number 57
Ndio hivi! Basi na wayaonje maji ya moto na ya usaha!
وَآخَرُ مِن شَكْلِهِ أَزْوَاجٌSorah Sad ( The Letter Sad ) Verse Number 58
Na adhabu nyenginezo za namna hii.
هَذَا فَوْجٌ مُّقْتَحِمٌ مَّعَكُمْ لا مَرْحَبًا بِهِمْ إِنَّهُمْ صَالُوا النَّارِSorah Sad ( The Letter Sad ) Verse Number 59
Hili ndilo kundi litakalo ingia pamoja nanyi. Hapana makaribisho mema kwao. Hakika hao wanaingia Motoni.
قَالُوا بَلْ أَنتُمْ لا مَرْحَبًا بِكُمْ أَنتُمْ قَدَّمْتُمُوهُ لَنَا فَبِئْسَ الْقَرَارُSorah Sad ( The Letter Sad ) Verse Number 60
Waseme: Lakini nyinyi! Hamna mapokezi mazuri! Nyinyi ndio mlio tusabibisha haya, napo ni pahala paovu kabisa!
قَالُوا رَبَّنَا مَن قَدَّمَ لَنَا هَذَا فَزِدْهُ عَذَابًا ضِعْفًا فِي النَّارِSorah Sad ( The Letter Sad ) Verse Number 61
Waseme: Mola wetu Mlezi! Aliye tusabibisha haya mzidishie adhabu mara mbili Motoni.
وَقَالُوا مَا لَنَا لا نَرَى رِجَالاً كُنَّا نَعُدُّهُم مِّنَ الأَشْرَارِSorah Sad ( The Letter Sad ) Verse Number 62
Watasema: Tuna nini hata hatuwaoni wale watu ambao tukiwahisabu ndio katika waovu?
أَتَّخَذْنَاهُمْ سِخْرِيًّا أَمْ زَاغَتْ عَنْهُمُ الأَبْصَارُSorah Sad ( The Letter Sad ) Verse Number 63
Tulikosea tulipo wafanyia maskhara, au macho yetu tu hayawaoni?
إِنَّ ذَلِكَ لَحَقٌّ تَخَاصُمُ أَهْلِ النَّارِSorah Sad ( The Letter Sad ) Verse Number 64
Hakika hayo bila ya shaka ndiyo makhasimiano ya watu wa Motoni.
قُلْ إِنَّمَا أَنَا مُنذِرٌ وَمَا مِنْ إِلَهٍ إِلاَّ اللَّهُ الْوَاحِدُ الْقَهَّارُSorah Sad ( The Letter Sad ) Verse Number 65
Sema: Hakika mimi ni mwonyaji tu; na hapana mungu ila Mwenyezi Mungu Mmoja, Mtenda nguvu,
رَبُّ السَّمَاوَاتِ وَالأَرْضِ وَمَا بَيْنَهُمَا الْعَزِيزُ الْغَفَّارُSorah Sad ( The Letter Sad ) Verse Number 66
Mola Mlezi wa mbingu na ardhi na viliomo baina yake, Mwenye nguvu, Mwenye kusamehe.
قُلْ هُوَ نَبَأٌ عَظِيمٌSorah Sad ( The Letter Sad ) Verse Number 67
Sema: Hii ni khabari kubwa kabisa.
أَنتُمْ عَنْهُ مُعْرِضُونَSorah Sad ( The Letter Sad ) Verse Number 68
Ambayo nyinyi mnaipuuza.
مَا كَانَ لِي مِنْ عِلْمٍ بِالْمَلَإِ الأَعْلَى إِذْ يَخْتَصِمُونَSorah Sad ( The Letter Sad ) Verse Number 69
Sikuwa na ilimu ya mambo ya viumbe wakuu watukufu walipo kuwa wakishindana.
إِن يُوحَى إِلَيَّ إِلاَّ أَنَّمَا أَنَا نَذِيرٌ مُّبِينٌSorah Sad ( The Letter Sad ) Verse Number 70
Haikufunuliwa kwangu isipo kuwa ya kwamba hakika mimi ni mwonyaji dhaahiri.
إِذْ قَالَ رَبُّكَ لِلْمَلائِكَةِ إِنِّي خَالِقٌ بَشَرًا مِن طِينٍSorah Sad ( The Letter Sad ) Verse Number 71
Mola wako Mlezi alipo waambia Malaika: Hakika Mimi nitaumba mtu kutokana na udongo.
فَإِذَا سَوَّيْتُهُ وَنَفَخْتُ فِيهِ مِن رُّوحِي فَقَعُوا لَهُ سَاجِدِينَSorah Sad ( The Letter Sad ) Verse Number 72
Na nitakapo mkamilisha na kumpulizia roho inayo tokana nami, basi muangukieni kwa kumt'ii.
فَسَجَدَ الْمَلائِكَةُ كُلُّهُمْ أَجْمَعُونَSorah Sad ( The Letter Sad ) Verse Number 73
Basi Malaika wakat'ii wote pamoja.
إِلاَّ إِبْلِيسَ اسْتَكْبَرَ وَكَانَ مِنْ الْكَافِرِينَSorah Sad ( The Letter Sad ) Verse Number 74
Isipo kuwa Iblisi; alijivuna na akawa katika makafiri.
قَالَ يَا إِبْلِيسُ مَا مَنَعَكَ أَن تَسْجُدَ لِمَا خَلَقْتُ بِيَدَيَّ أَسْتَكْبَرْتَ أَمْ كُنتَ مِنَ الْعَالِينَSorah Sad ( The Letter Sad ) Verse Number 75
Mwenyezi Mungu akamwambia: Ewe Iblisi! Kipi kilicho kuzuia kumt'ii yule niliye muumba kwa mikono yangu? Je! Umejiona mkubwa, au umekuwa katika wakuu kweli?
قَالَ أَنَا خَيْرٌ مِّنْهُ خَلَقْتَنِي مِن نَّارٍ وَخَلَقْتَهُ مِن طِينٍSorah Sad ( The Letter Sad ) Verse Number 76
Akasema: Mimi ni bora kuliko yeye. Umeniumba kwa moto, na yeye umemuumba kwa udongo.
قَالَ فَاخْرُجْ مِنْهَا فَإِنَّكَ رَجِيمٌSorah Sad ( The Letter Sad ) Verse Number 77
Akasema: Basi toka humo, kwani hakika wewe umelaanika.
وَإِنَّ عَلَيْكَ لَعْنَتِي إِلَى يَوْمِ الدِّينِSorah Sad ( The Letter Sad ) Verse Number 78
Na hakika laana yangu itakuwa juu yako mpaka Siku ya Malipo.
قَالَ رَبِّ فَأَنظِرْنِي إِلَى يَوْمِ يُبْعَثُونَSorah Sad ( The Letter Sad ) Verse Number 79
Akasema: Mola wangu Mlezi! Nipe muhula mpaka siku watayo fufuliwa viumbe.
قَالَ فَإِنَّكَ مِنَ الْمُنظَرِينَSorah Sad ( The Letter Sad ) Verse Number 80
Mwenyezi Mungu akasema: Basi umekwisha kuwa miongoni mwa walio pewa muhula,
إِلَى يَوْمِ الْوَقْتِ الْمَعْلُومِSorah Sad ( The Letter Sad ) Verse Number 81
Mpaka siku ya wakati maalumu.
قَالَ فَبِعِزَّتِكَ لَأُغْوِيَنَّهُمْ أَجْمَعِينَSorah Sad ( The Letter Sad ) Verse Number 82
Akasema (Iblisi): Naapa kwa utukufu wako, bila ya shaka nitawapoteza wote,
إِلاَّ عِبَادَكَ مِنْهُمُ الْمُخْلَصِينَSorah Sad ( The Letter Sad ) Verse Number 83
Isipo kuwa wale waja wako miongoni mwao walio khitariwa.
قَالَ فَالْحَقُّ وَالْحَقَّ أَقُولُSorah Sad ( The Letter Sad ) Verse Number 84
Akasema: Haki! Na haki ninaisema.
لَأَمْلَأَنَّ جَهَنَّمَ مِنكَ وَمِمَّن تَبِعَكَ مِنْهُمْ أَجْمَعِينَSorah Sad ( The Letter Sad ) Verse Number 85
Bila ya shaka nitaijaza Jahannamu kwa wewe na kwa hao wote wenye kukufuata miongoni mwao.
قُلْ مَا أَسْأَلُكُمْ عَلَيْهِ مِنْ أَجْرٍ وَمَا أَنَا مِنَ الْمُتَكَلِّفِينَSorah Sad ( The Letter Sad ) Verse Number 86
Sema (Ewe Mtume): Sikuombeni ujira juu ya haya, wala mimi si katika wadanganyifu.
إِنْ هُوَ إِلاَّ ذِكْرٌ لِّلْعَالَمِينَSorah Sad ( The Letter Sad ) Verse Number 87
Hayakuwa haya ila ni mawaidha kwa walimwengu wote.
وَلَتَعْلَمُنَّ نَبَأَهُ بَعْدَ حِينٍSorah Sad ( The Letter Sad ) Verse Number 88
Na bila ya shaka mtajua khabari zake baada ya muda.