Swahili
Sorah Al-Mu'minoon ( The Believers )

Verses Number 118

قَدْ أَفْلَحَ الْمُؤْمِنُونَSorah Al-Mu'minoon ( The Believers ) Verse Number 1
HAKIKA wamefanikiwa Waumini,
الَّذِينَ هُمْ فِي صَلاتِهِمْ خَاشِعُونَSorah Al-Mu'minoon ( The Believers ) Verse Number 2
Ambao ni wanyenyekevu katika Sala zao,
وَالَّذِينَ هُمْ عَنِ اللَّغْوِ مُعْرِضُونَSorah Al-Mu'minoon ( The Believers ) Verse Number 3
Na ambao hujiepusha na mambo ya upuuzi,
وَالَّذِينَ هُمْ لِلزَّكَاةِ فَاعِلُونَSorah Al-Mu'minoon ( The Believers ) Verse Number 4
Na ambao wanatoa Zaka,
وَالَّذِينَ هُمْ لِفُرُوجِهِمْ حَافِظُونَSorah Al-Mu'minoon ( The Believers ) Verse Number 5
Na ambao wanazilinda tupu zao,
إِلاَّ عَلَى أَزْوَاجِهِمْ أَوْ مَا مَلَكَتْ أَيْمَانُهُمْ فَإِنَّهُمْ غَيْرُ مَلُومِينَSorah Al-Mu'minoon ( The Believers ) Verse Number 6
Isipo kuwa kwa wake zao au kwa iliyo wamiliki mikono yao ya kulia. Kwani hao si wenye kulaumiwa.
فَمَنِ ابْتَغَى وَرَاء ذَلِكَ فَأُولَئِكَ هُمُ الْعَادُونَSorah Al-Mu'minoon ( The Believers ) Verse Number 7
Lakini anaye taka kinyume cha haya, basi hao ndio warukao mipaka.
وَالَّذِينَ هُمْ لِأَمَانَاتِهِمْ وَعَهْدِهِمْ رَاعُونَSorah Al-Mu'minoon ( The Believers ) Verse Number 8
Na ambao wanazitimiza amana zao na ahadi zao,
وَالَّذِينَ هُمْ عَلَى صَلَوَاتِهِمْ يُحَافِظُونَSorah Al-Mu'minoon ( The Believers ) Verse Number 9
Na ambao Sala zao wanazihifadhi -
أُوْلَئِكَ هُمُ الْوَارِثُونَSorah Al-Mu'minoon ( The Believers ) Verse Number 10
Hao ndio warithi,
الَّذِينَ يَرِثُونَ الْفِرْدَوْسَ هُمْ فِيهَا خَالِدُونَSorah Al-Mu'minoon ( The Believers ) Verse Number 11
Ambao watairithi Pepo ya Firdausi, wadumu humo.
وَلَقَدْ خَلَقْنَا الإِنسَانَ مِن سُلالَةٍ مِّن طِينٍSorah Al-Mu'minoon ( The Believers ) Verse Number 12
Na kwa yakini tumemuumba mtu kutokana na asli ya udongo.
ثُمَّ جَعَلْنَاهُ نُطْفَةً فِي قَرَارٍ مَّكِينٍSorah Al-Mu'minoon ( The Believers ) Verse Number 13
Kisha tukamjaalia awe tone ya mbegu ya uzazi katika kalio madhubuti.
ثُمَّ خَلَقْنَا النُّطْفَةَ عَلَقَةً فَخَلَقْنَا الْعَلَقَةَ مُضْغَةً فَخَلَقْنَا الْمُضْغَةَ عِظَامًا فَكَسَوْنَا الْعِظَامَ لَحْمًا ثُمَّ أَنشَأْنَاهُ خَلْقًا آخَرَ فَتَبَارَكَ اللَّهُ أَحْسَنُ الْخَالِقِينَSorah Al-Mu'minoon ( The Believers ) Verse Number 14
Kisha tukaiumba tone kuwa damu iliyo ganda, na tukaiumba damu kuwa pande la nyama, kisha tukaliumba pande la nyama kuwa mifupa, na mifupa tukaivika nyama. Kisha tukamfanya kiumbe mwengine. Basi ametukuka Mwenyezi Mungu Mbora wa waumbaji.
ثُمَّ إِنَّكُمْ بَعْدَ ذَلِكَ لَمَيِّتُونَSorah Al-Mu'minoon ( The Believers ) Verse Number 15
Kisha hakika nyinyi baada ya hayo mtakufa.
ثُمَّ إِنَّكُمْ يَوْمَ الْقِيَامَةِ تُبْعَثُونَSorah Al-Mu'minoon ( The Believers ) Verse Number 16
Kisha hakika nyinyi Siku ya Kiyama mtafufuliwa.
وَلَقَدْ خَلَقْنَا فَوْقَكُمْ سَبْعَ طَرَائِقَ وَمَا كُنَّا عَنِ الْخَلْقِ غَافِلِينَSorah Al-Mu'minoon ( The Believers ) Verse Number 17
Na kwa yakini tumeziumba juu yenu njia saba. Nasi hatukuwa wenye kughafilika na viumbe.
وَأَنزَلْنَا مِنَ السَّمَاء مَاء بِقَدَرٍ فَأَسْكَنَّاهُ فِي الأَرْضِ وَإِنَّا عَلَى ذَهَابٍ بِهِ لَقَادِرُونَSorah Al-Mu'minoon ( The Believers ) Verse Number 18
Na tumeteremsha kutoka mbinguni maji kwa kiasi na tukayatuliza katika ardhi. Na hakika Sisi tunaweza kuyaondoa.
فَأَنشَأْنَا لَكُم بِهِ جَنَّاتٍ مِّن نَّخِيلٍ وَأَعْنَابٍ لَّكُمْ فِيهَا فَوَاكِهُ كَثِيرَةٌ وَمِنْهَا تَأْكُلُونَSorah Al-Mu'minoon ( The Believers ) Verse Number 19
Kwa maji hayo tukakufanyieni bustani za mitende na mizabibu, mnapata humo matunda mengi, na katika hayo mnakula;
وَشَجَرَةً تَخْرُجُ مِن طُورِ سَيْنَاءَ تَنبُتُ بِالدُّهْنِ وَصِبْغٍ لِّلْآكِلِينَSorah Al-Mu'minoon ( The Believers ) Verse Number 20
Na mti utokao katika mlima wa Sinai, unatoa mafuta na kuwa kitoweo kwa walao.
وَإِنَّ لَكُمْ فِي الأَنْعَامِ لَعِبْرَةً نُّسْقِيكُم مِّمَّا فِي بُطُونِهَا وَلَكُمْ فِيهَا مَنَافِعُ كَثِيرَةٌ وَمِنْهَا تَأْكُلُونَSorah Al-Mu'minoon ( The Believers ) Verse Number 21
Na hakika mnayo mazingatio makubwa katika nyama hoa - tunakunywesheni katika vile viliomo matumboni mwao, na nyinyi mnapata katika hao manufaa mengi, na pia mnawala.
وَعَلَيْهَا وَعَلَى الْفُلْكِ تُحْمَلُونَSorah Al-Mu'minoon ( The Believers ) Verse Number 22
Na juu yao na juu ya marikebu mnabebwa.
وَلَقَدْ أَرْسَلْنَا نُوحًا إِلَى قَوْمِهِ فَقَالَ يَا قَوْمِ اعْبُدُوا اللَّهَ مَا لَكُم مِّنْ إِلَهٍ غَيْرُهُ أَفَلا تَتَّقُونَSorah Al-Mu'minoon ( The Believers ) Verse Number 23
Na hakika tulimtuma Nuhu kwa watu wake, akasema: Enyi watu wangu! Muabuduni Mwenyezi Mungu. Nyinyi hamna mungu asiye kuwa Yeye. Basi je! Hamwogopi?
فَقَالَ الْمَلَأُ الَّذِينَ كَفَرُوا مِن قَوْمِهِ مَا هَذَا إِلاَّ بَشَرٌ مِّثْلُكُمْ يُرِيدُ أَن يَتَفَضَّلَ عَلَيْكُمْ وَلَوْ شَاء اللَّهُ لَأَنزَلَ مَلائِكَةً مَّا سَمِعْنَا بِهَذَا فِي آبَائِنَا الأَوَّلِينَSorah Al-Mu'minoon ( The Believers ) Verse Number 24
Walisema wale wakuu walio kufuru katika watu wake: Huyu si chochote ila ni mtu tu kama nyinyi. Anataka kujipa ubora juu yenu. Na lau kuwa Mwenyezi Mungu amependa basi yakini angeli teremsha Malaika. Hatukusikia haya kwa baba zetu wa zamani.
إِنْ هُوَ إِلاَّ رَجُلٌ بِهِ جِنَّةٌ فَتَرَبَّصُوا بِهِ حَتَّى حِينٍSorah Al-Mu'minoon ( The Believers ) Verse Number 25
Huyu si lolote ila ni mtu mwenye wazimu. Basi mngojeeni tu kwa muda.
قَالَ رَبِّ انصُرْنِي بِمَا كَذَّبُونِSorah Al-Mu'minoon ( The Believers ) Verse Number 26
Akasema (Nuhu): Mola wangu Mlezi! Ninusuru kwa kuwa wamenikanusha.
فَأَوْحَيْنَا إِلَيْهِ أَنِ اصْنَعِ الْفُلْكَ بِأَعْيُنِنَا وَوَحْيِنَا فَإِذَا جَاءَ أَمْرُنَا وَفَارَ التَّنُّورُ فَاسْلُكْ فِيهَا مِن كُلٍّ زَوْجَيْنِ اثْنَيْنِ وَأَهْلَكَ إِلاَّ مَن سَبَقَ عَلَيْهِ الْقَوْلُ مِنْهُمْ وَلا تُخَاطِبْنِي فِي الَّذِينَ ظَلَمُوا إِنَّهُم مُّغْرَقُونَSorah Al-Mu'minoon ( The Believers ) Verse Number 27
Tukampa wahyi: Unda jahazi mbele ya macho yetu na uwongozi wetu! Basi itapo fika amri yetu na ikafurika tanuri, hapo waingize ndani yake wa kila namna dume na jike, na ahali zako, isipo kuwa yule ambaye katika wao juu yake imekwisha tangulia kauli. Wala usinitajie hao walio dhulumu. Kwani hao bila ya shaka watazamishwa.
فَإِذَا اسْتَوَيْتَ أَنتَ وَمَن مَّعَكَ عَلَى الْفُلْكِ فَقُلِ الْحَمْدُ لِلَّهِ الَّذِي نَجَّانَا مِنَ الْقَوْمِ الظَّالِمِينَSorah Al-Mu'minoon ( The Believers ) Verse Number 28
Basi utakapo tulia wewe na walio pamoja nawe humo marikebuni, sema: Alhamdulillahi Sifa zote njema ni za Mwenyezi Mungu, aliye tuokoa na watu madhaalimu!
وَقُل رَّبِّ أَنزِلْنِي مُنزَلا مُّبَارَكًا وَأَنتَ خَيْرُ الْمُنزِلِينَSorah Al-Mu'minoon ( The Believers ) Verse Number 29
Na sema: Mola wangu Mlezi! Niteremshe mteremsho wenye baraka, na Wewe ni Mbora wa wateremshaji.
إِنَّ فِي ذَلِكَ لَآيَاتٍ وَإِن كُنَّا لَمُبْتَلِينَSorah Al-Mu'minoon ( The Believers ) Verse Number 30
Hakika katika hayo yapo mazingatio. Na kwa yakini Sisi ni wenye kuwafanyia mtihani.
ثُمَّ أَنشَأْنَا مِن بَعْدِهِمْ قَرْنًا آخَرِينَSorah Al-Mu'minoon ( The Believers ) Verse Number 31
Kisha baada yao tukaanzisha kizazi kingine.
فَأَرْسَلْنَا فِيهِمْ رَسُولا مِنْهُمْ أَنِ اعْبُدُوا اللَّهَ مَا لَكُم مِّنْ إِلَهٍ غَيْرُهُ أَفَلا تَتَّقُونَSorah Al-Mu'minoon ( The Believers ) Verse Number 32
Tukawapelekea Mtume miongoni mwao, kuwaambia: Muabuduni Mwenyezi Mungu! Hamna mungu asiye kuwa Yeye. Jee, hamwogopi?
وَقَالَ الْمَلَأُ مِن قَوْمِهِ الَّذِينَ كَفَرُوا وَكَذَّبُوا بِلِقَاء الآخِرَةِ وَأَتْرَفْنَاهُمْ فِي الْحَيَاةِ الدُّنْيَا مَا هَذَا إِلاَّ بَشَرٌ مِّثْلُكُمْ يَأْكُلُ مِمَّا تَأْكُلُونَ مِنْهُ وَيَشْرَبُ مِمَّا تَشْرَبُونَSorah Al-Mu'minoon ( The Believers ) Verse Number 33
Na wakubwa katika watu wake walio kufuru na wakakanusha mkutano wa Akhera, na tukawadekeza kwa starehe katika maisha ya dunia, walisema: Huyu si chochote ila ni binaadamu kama nyinyi; anakula mlacho, na anakunywa mnywacho.
وَلَئِنْ أَطَعْتُم بَشَرًا مِثْلَكُمْ إِنَّكُمْ إِذًا لَّخَاسِرُونَSorah Al-Mu'minoon ( The Believers ) Verse Number 34
Na nyinyi mkimt'ii mtu kama nyinyi basi hakika mtakuwa khasarani.
أَيَعِدُكُمْ أَنَّكُمْ إِذَا مِتُّمْ وَكُنتُمْ تُرَابًا وَعِظَامًا أَنَّكُم مُّخْرَجُونَSorah Al-Mu'minoon ( The Believers ) Verse Number 35
Hivyo anakuahidini ati ya kwamba mtakapo kufa na mkawa udongo na mifupa kuwa mtatolewa?
هَيْهَاتَ هَيْهَاتَ لِمَا تُوعَدُونَSorah Al-Mu'minoon ( The Believers ) Verse Number 36
Hayawi! Hayawi hayo mnayo ahidiwa.
إِنْ هِيَ إِلاَّ حَيَاتُنَا الدُّنْيَا نَمُوتُ وَنَحْيَا وَمَا نَحْنُ بِمَبْعُوثِينَSorah Al-Mu'minoon ( The Believers ) Verse Number 37
Hapana ila uhai wetu wa duniani tu, tunakufa na kuishi basi. Wala sisi hatutafufuliwa.
إِنْ هُوَ إِلاَّ رَجُلٌ افْتَرَى عَلَى اللَّهِ كَذِبًا وَمَا نَحْنُ لَهُ بِمُؤْمِنِينَSorah Al-Mu'minoon ( The Believers ) Verse Number 38
Huyu si lolote ila ni mtu anaye mzulia Mwenyezi Mungu uwongo, wala sisi sio wa kumuamini.
قَالَ رَبِّ انصُرْنِي بِمَا كَذَّبُونِSorah Al-Mu'minoon ( The Believers ) Verse Number 39
Akasema: Mola wangu Mlezi! Ninusuru kwa sababu wananikanusha.
قَالَ عَمَّا قَلِيلٍ لَيُصْبِحُنَّ نَادِمِينَSorah Al-Mu'minoon ( The Believers ) Verse Number 40
(Mwenyezi Mungu) akasema: Baada ya muda mchache watakuwa wenye kujuta.
فَأَخَذَتْهُمُ الصَّيْحَةُ بِالْحَقِّ فَجَعَلْنَاهُمْ غُثَاءً فَبُعْدًا لِّلْقَوْمِ الظَّالِمِينَSorah Al-Mu'minoon ( The Believers ) Verse Number 41
Basi ukawanyakua ukelele kwa haki, na tukawafanya kama takataka zinazo elea juu ya maji. Ikapotelea mbali kaumu ya madhaalimu!
ثُمَّ أَنشَأْنَا مِن بَعْدِهِمْ قُرُونًا آخَرِينَSorah Al-Mu'minoon ( The Believers ) Verse Number 42
Kisha tukaleta baada yao vizazi vingine.
مَا تَسْبِقُ مِنْ أُمَّةٍ أَجَلَهَا وَمَا يَسْتَأْخِرُونَSorah Al-Mu'minoon ( The Believers ) Verse Number 43
Hapana umma uwezao kutanguliza ajali yake wala kuikawiza.
ثُمَّ أَرْسَلْنَا رُسُلَنَا تَتْرَا كُلَّ مَا جَاءَ أُمَّةً رَّسُولُهَا كَذَّبُوهُ فَأَتْبَعْنَا بَعْضَهُم بَعْضًا وَجَعَلْنَاهُمْ أَحَادِيثَ فَبُعْدًا لِّقَوْمٍ لّا يُؤْمِنُونَSorah Al-Mu'minoon ( The Believers ) Verse Number 44
Kisha tukawatuma Mitume wetu, mmoja baada ya mmoja. Kila umma alipo wafikia Mtume wao walimkanusha. Tukawafuatanisha hawa baada ya hawa, na tukawafanya ni hadithi za kusimuliwa. Wakapotelea mbali watu wasio amini.
ثُمَّ أَرْسَلْنَا مُوسَى وَأَخَاهُ هَارُونَ بِآيَاتِنَا وَسُلْطَانٍ مُّبِينٍSorah Al-Mu'minoon ( The Believers ) Verse Number 45
Kisha tukamtuma Musa na nduguye, Haaruni, pamoja na ishara zetu na hoja zilizo wazi.
إِلَى فِرْعَوْنَ وَمَلَئِهِ فَاسْتَكْبَرُوا وَكَانُوا قَوْمًا عَالِينَSorah Al-Mu'minoon ( The Believers ) Verse Number 46
Kumwendea Firauni na wakuu wake. Lakini walijivuna, nao walikuwa watu majeuri.
فَقَالُوا أَنُؤْمِنُ لِبَشَرَيْنِ مِثْلِنَا وَقَوْمُهُمَا لَنَا عَابِدُونَSorah Al-Mu'minoon ( The Believers ) Verse Number 47
Wakasema: Je, tuwaamini wanaadamu wawili hawa kama sisi, na ambao watu wao ni watumwa wetu?
فَكَذَّبُوهُمَا فَكَانُوا مِنَ الْمُهْلَكِينَSorah Al-Mu'minoon ( The Believers ) Verse Number 48
Basi wakawakanusha, na wakawa miongoni mwa walio angamizwa.
وَلَقَدْ آتَيْنَا مُوسَى الْكِتَابَ لَعَلَّهُمْ يَهْتَدُونَSorah Al-Mu'minoon ( The Believers ) Verse Number 49
Na hakika tulimpa Musa Kitabu ili wapate kuongoka.
وَجَعَلْنَا ابْنَ مَرْيَمَ وَأُمَّهُ آيَةً وَآوَيْنَاهُمَا إِلَى رَبْوَةٍ ذَاتِ قَرَارٍ وَمَعِينٍSorah Al-Mu'minoon ( The Believers ) Verse Number 50
Na tukamfanya mwana wa Mariamu na mama yake kuwa ni Ishara, na tukawapa makimbilio kwenda mahali palipo inuka penye utulivu na chemchem za maji.
يَا أَيُّهَا الرُّسُلُ كُلُوا مِنَ الطَّيِّبَاتِ وَاعْمَلُوا صَالِحًا إِنِّي بِمَا تَعْمَلُونَ عَلِيمٌSorah Al-Mu'minoon ( The Believers ) Verse Number 51
Enyi Mitume! Kuleni vyakula vizuri na tendeni mema. Hakika Mimi ni Mjuzi wa mnayo yatenda.
وَإِنَّ هَذِهِ أُمَّتُكُمْ أُمَّةً وَاحِدَةً وَأَنَا رَبُّكُمْ فَاتَّقُونِSorah Al-Mu'minoon ( The Believers ) Verse Number 52
Na kwa yakini huu Umma wenu ni Umma mmoja, na Mimi ni Mola wenu Mlezi, basi nicheni Mimi.
فَتَقَطَّعُوا أَمْرَهُم بَيْنَهُمْ زُبُرًا كُلُّ حِزْبٍ بِمَا لَدَيْهِمْ فَرِحُونَSorah Al-Mu'minoon ( The Believers ) Verse Number 53
Lakini walikatiana jambo lao mapande mbali mbali. Kila kundi likifurahia kwa waliyo nayo.
فَذَرْهُمْ فِي غَمْرَتِهِمْ حَتَّى حِينٍSorah Al-Mu'minoon ( The Believers ) Verse Number 54
Basi waache katika ghafla yao kwa muda.
أَيَحْسَبُونَ أَنَّمَا نُمِدُّهُم بِهِ مِن مَّالٍ وَبَنِينَSorah Al-Mu'minoon ( The Believers ) Verse Number 55
Je! Wanadhani ya kuwa kwa vile tunavyo wapa mali na watoto
نُسَارِعُ لَهُمْ فِي الْخَيْرَاتِ بَل لّا يَشْعُرُونَSorah Al-Mu'minoon ( The Believers ) Verse Number 56
Ndio tunawahimizia kheri? Lakini wenyewe hawatambui.
إِنَّ الَّذِينَ هُم مِّنْ خَشْيَةِ رَبِّهِم مُّشْفِقُونَSorah Al-Mu'minoon ( The Believers ) Verse Number 57
Kwa hakika hao ambao kwa kumwogopa Mola wao Mlezi wananyenyekea,
وَالَّذِينَ هُم بِآيَاتِ رَبِّهِمْ يُؤْمِنُونَSorah Al-Mu'minoon ( The Believers ) Verse Number 58
Na wale ambao Ishara za Mola wao Mlezi wanaziamini,
وَالَّذِينَ هُم بِرَبِّهِمْ لا يُشْرِكُونَSorah Al-Mu'minoon ( The Believers ) Verse Number 59
Na wale ambao Mola wao Mlezi hawamshirikishi,
وَالَّذِينَ يُؤْتُونَ مَا آتَوا وَّقُلُوبُهُمْ وَجِلَةٌ أَنَّهُمْ إِلَى رَبِّهِمْ رَاجِعُونَSorah Al-Mu'minoon ( The Believers ) Verse Number 60
Na wale ambao wanatoa walicho pewa, na hali nyoyo zao zinagopa kwa kuwa watarejea kwa Mola wao Mlezi,
أُوْلَئِكَ يُسَارِعُونَ فِي الْخَيْرَاتِ وَهُمْ لَهَا سَابِقُونَSorah Al-Mu'minoon ( The Believers ) Verse Number 61
Basi wote hao ndio wanao kimbilia katika mambo ya kheri, na ndio watakao tangulia kuyafikia.
وَلا نُكَلِّفُ نَفْسًا إِلاَّ وُسْعَهَا وَلَدَيْنَا كِتَابٌ يَنطِقُ بِالْحَقِّ وَهُمْ لا يُظْلَمُونَSorah Al-Mu'minoon ( The Believers ) Verse Number 62
Na hatuilazimishi nafsi ila kwa kadri ya uwezo wake. Na tunacho kitabu kisemacho kweli. Nao hawatadhulumiwa.
بَلْ قُلُوبُهُمْ فِي غَمْرَةٍ مِّنْ هَذَا وَلَهُمْ أَعْمَالٌ مِن دُونِ ذَلِكَ هُمْ لَهَا عَامِلُونَSorah Al-Mu'minoon ( The Believers ) Verse Number 63
Lakini nyoyo zao zimeghafilika na hayo, na wanavyo vitendo vinginevyo wanavyo vifanya.
حَتَّى إِذَا أَخَذْنَا مُتْرَفِيهِم بِالْعَذَابِ إِذَا هُمْ يَجْأَرُونَSorah Al-Mu'minoon ( The Believers ) Verse Number 64
Hata tutakapo watia katika adhabu wale walio dekezwa kwa starehe kati yao, hapo ndipo watapo yayatika.
لا تَجْأَرُوا الْيَوْمَ إِنَّكُم مِّنَّا لا تُنصَرُونَSorah Al-Mu'minoon ( The Believers ) Verse Number 65
Msiyayatike leo! Hakika nyinyi hamtanusurika nasi.
قَدْ كَانَتْ آيَاتِي تُتْلَى عَلَيْكُمْ فَكُنتُمْ عَلَى أَعْقَابِكُمْ تَنكِصُونَSorah Al-Mu'minoon ( The Believers ) Verse Number 66
Hakika zilikuwa Aya zangu mkisomewa, nanyi mkirudi nyuma juu ya visigino vyenu,
مُسْتَكْبِرِينَ بِهِ سَامِرًا تَهْجُرُونَSorah Al-Mu'minoon ( The Believers ) Verse Number 67
Na huku mkitakabari na usiku mkiizungumza (Qur'ani) kwa dharau.
أَفَلَمْ يَدَّبَّرُوا الْقَوْلَ أَمْ جَاءَهُم مَّا لَمْ يَأْتِ آبَاءَهُمُ الأَوَّلِينَSorah Al-Mu'minoon ( The Believers ) Verse Number 68
Je, hawakuifikiri kauli, au yamewajia yasiyo wafikia baba zao wa zamani?
أَمْ لَمْ يَعْرِفُوا رَسُولَهُمْ فَهُمْ لَهُ مُنكِرُونَSorah Al-Mu'minoon ( The Believers ) Verse Number 69
Au hawakumjua Mtume wao, ndio maana wanamkataa?
أَمْ يَقُولُونَ بِهِ جِنَّةٌ بَلْ جَاءَهُم بِالْحَقِّ وَأَكْثَرُهُمْ لِلْحَقِّ كَارِهُونَSorah Al-Mu'minoon ( The Believers ) Verse Number 70
Au wanasema: Ana wazimu? Bali amewajia kwa Haki, na wengi wao wanaichukia Haki.
وَلَوِ اتَّبَعَ الْحَقُّ أَهْوَاءهُمْ لَفَسَدَتِ السَّمَاوَاتُ وَالأَرْضُ وَمَن فِيهِنَّ بَلْ أَتَيْنَاهُم بِذِكْرِهِمْ فَهُمْ عَن ذِكْرِهِم مُّعْرِضُونَSorah Al-Mu'minoon ( The Believers ) Verse Number 71
Na lau kuwa Haki ingeli fuata matamanio yao, basi zingeli haribika mbingu na ardhi na waliomo ndani. Bali tumewaletea ukumbusho wao, nao wanajitenga mbali na ukumbusho wao.
أَمْ تَسْأَلُهُمْ خَرْجًا فَخَرَاجُ رَبِّكَ خَيْرٌ وَهُوَ خَيْرُ الرَّازِقِينَSorah Al-Mu'minoon ( The Believers ) Verse Number 72
Au unawaomba ujira? Lakini ujira wa Mola wako Mlezi ni bora, na Yeye ndiye Mbora wa wanao ruzuku.
وَإِنَّكَ لَتَدْعُوهُمْ إِلَى صِرَاطٍ مُّسْتَقِيمٍSorah Al-Mu'minoon ( The Believers ) Verse Number 73
Na kwa yakini wewe unawaita kwenye Njia Iliyo Nyooka.
وَإِنَّ الَّذِينَ لا يُؤْمِنُونَ بِالآخِرَةِ عَنِ الصِّرَاطِ لَنَاكِبُونَSorah Al-Mu'minoon ( The Believers ) Verse Number 74
Na hakika wale wasio iamini Akhera wanajitenga na Njia hiyo.
وَلَوْ رَحِمْنَاهُمْ وَكَشَفْنَا مَا بِهِم مِّن ضُرٍّ لَّلَجُّوا فِي طُغْيَانِهِمْ يَعْمَهُونَSorah Al-Mu'minoon ( The Believers ) Verse Number 75
Na lau tungeli warehemu na tukawaondolea shida waliyo nayo bila ya shaka wangeli endelea katika upotofu wao vile vile, wakitangatanga.
وَلَقَدْ أَخَذْنَاهُم بِالْعَذَابِ فَمَا اسْتَكَانُوا لِرَبِّهِمْ وَمَا يَتَضَرَّعُونَSorah Al-Mu'minoon ( The Believers ) Verse Number 76
Na hakika tuliwatia adhabu kali; lakini hawakuelekea kwa Mola wao Mlezi wala hawakunyenyekea.
حَتَّى إِذَا فَتَحْنَا عَلَيْهِم بَابًا ذَا عَذَابٍ شَدِيدٍ إِذَا هُمْ فِيهِ مُبْلِسُونَSorah Al-Mu'minoon ( The Believers ) Verse Number 77
Mpaka tulipo wafungulia mlango wa adhabu kali, hapo ndipo wakawa wenye kukata tamaa.
وَهُوَ الَّذِي أَنشَأَ لَكُمُ السَّمْعَ وَالأَبْصَارَ وَالأَفْئِدَةَ قَلِيلا مَّا تَشْكُرُونَSorah Al-Mu'minoon ( The Believers ) Verse Number 78
Na Yeye ndiye aliye kuumbieni kusikia na kuona na nyoyo za kufahamu. Ni kuchache mno kushukuru kwenu.
وَهُوَ الَّذِي ذَرَأَكُمْ فِي الأَرْضِ وَإِلَيْهِ تُحْشَرُونَSorah Al-Mu'minoon ( The Believers ) Verse Number 79
Na Yeye ndiye aliye kuenezeni katika ardhi, na kwake Yeye mtakusanywa.
وَهُوَ الَّذِي يُحْيِي وَيُمِيتُ وَلَهُ اخْتِلافُ اللَّيْلِ وَالنَّهَارِ أَفَلا تَعْقِلُونَSorah Al-Mu'minoon ( The Believers ) Verse Number 80
Na Yeye ndiye anaye huisha na kufisha, na yake Yeye mabadiliko ya usiku na mchana. Basi je! Hamfahamu?
بَلْ قَالُوا مِثْلَ مَا قَالَ الأَوَّلُونَSorah Al-Mu'minoon ( The Believers ) Verse Number 81
Bali wanasema kama walivyo sema watu wa kwanza.
قَالُوا أَئِذَا مِتْنَا وَكُنَّا تُرَابًا وَعِظَامًا أَئِنَّا لَمَبْعُوثُونَSorah Al-Mu'minoon ( The Believers ) Verse Number 82
Walisema: Je! Tukisha kufa tukawa udongo na mifupa ndio tutafufuliwa?
لَقَدْ وُعِدْنَا نَحْنُ وَآبَاؤُنَا هَذَا مِن قَبْلُ إِنْ هَذَا إِلاَّ أَسَاطِيرُ الأَوَّلِينَSorah Al-Mu'minoon ( The Believers ) Verse Number 83
Tuliahidiwa haya sisi na baba zetu zamani. Hayakuwa haya ila ni visa vya uwongo vya watu wa zamani.
قُل لِّمَنِ الأَرْضُ وَمَن فِيهَا إِن كُنتُمْ تَعْلَمُونَSorah Al-Mu'minoon ( The Believers ) Verse Number 84
Sema: Ni ya nani ardhi na viliomo ndani yake, kama nyinyi mnajua?
سَيَقُولُونَ لِلَّهِ قُلْ أَفَلا تَذَكَّرُونَSorah Al-Mu'minoon ( The Believers ) Verse Number 85
Watasema: Ni vya Mwenyezi Mungu! Sema: Basi, je, hamkumbuki?
قُلْ مَن رَّبُّ السَّمَاوَاتِ السَّبْعِ وَرَبُّ الْعَرْشِ الْعَظِيمِSorah Al-Mu'minoon ( The Believers ) Verse Number 86
Sema: Ni nani Mola Mlezi wa mbingu saba na Mola Mlezi wa A'rshi Kuu?
سَيَقُولُونَ لِلَّهِ قُلْ أَفَلا تَتَّقُونَSorah Al-Mu'minoon ( The Believers ) Verse Number 87
Watasema: Ni vya Mwenyezi Mungu. Sema: Basi je, hamwogopi?
قُلْ مَن بِيَدِهِ مَلَكُوتُ كُلِّ شَيْءٍ وَهُوَ يُجِيرُ وَلا يُجَارُ عَلَيْهِ إِن كُنتُمْ تَعْلَمُونَSorah Al-Mu'minoon ( The Believers ) Verse Number 88
Sema: Ni nani mkononi mwake umo Ufalme wa kila kitu, naye ndiye anaye linda, wala hakilindwi asicho taka, kama mnajua?
سَيَقُولُونَ لِلَّهِ قُلْ فَأَنَّى تُسْحَرُونَSorah Al-Mu'minoon ( The Believers ) Verse Number 89
Watasema: (Ufalme huo) ni wa Mwenyezi Mungu. Sema: Basi vipi mnadanganyika?
بَلْ أَتَيْنَاهُم بِالْحَقِّ وَإِنَّهُمْ لَكَاذِبُونَSorah Al-Mu'minoon ( The Believers ) Verse Number 90
Bali tumewaletea Haki, na kwa yakini hao ni waongo.
مَا اتَّخَذَ اللَّهُ مِن وَلَدٍ وَمَا كَانَ مَعَهُ مِنْ إِلَهٍ إِذًا لَّذَهَبَ كُلُّ إِلَهٍ بِمَا خَلَقَ وَلَعَلا بَعْضُهُمْ عَلَى بَعْضٍ سُبْحَانَ اللَّهِ عَمَّا يَصِفُونَSorah Al-Mu'minoon ( The Believers ) Verse Number 91
Mwenyezi Mungu hana mwana yeyote, wala hanaye mungu mwengine. Inge kuwa hivyo basi kila mungu angeli chukua alivyo umba, na baadhi yao wangeli washinda wengine. Mwenyezi Mungu ameepukana na sifa wanazo msifu.
عَالِمِ الْغَيْبِ وَالشَّهَادَةِ فَتَعَالَى عَمَّا يُشْرِكُونَSorah Al-Mu'minoon ( The Believers ) Verse Number 92
Mjuzi wa siri na dhaahiri, na ametukuka juu ya hayo wanayo mshirikisha nayo.
قُل رَّبِّ إِمَّا تُرِيَنِّي مَا يُوعَدُونَSorah Al-Mu'minoon ( The Believers ) Verse Number 93
Sema: Mola wangu Mlezi! Ukinionyesha adhabu waliyo ahidiwa,
رَبِّ فَلا تَجْعَلْنِي فِي الْقَوْمِ الظَّالِمِينَSorah Al-Mu'minoon ( The Believers ) Verse Number 94
Mola wangu Mlezi! Usinijaalie katika watu madhaalimu hao.
وَإِنَّا عَلَى أَن نُّرِيَكَ مَا نَعِدُهُمْ لَقَادِرُونَSorah Al-Mu'minoon ( The Believers ) Verse Number 95
Na hakika Sisi ni waweza wa kukuonyeshsa tuliyo waahidi.
ادْفَعْ بِالَّتِي هِيَ أَحْسَنُ السَّيِّئَةَ نَحْنُ أَعْلَمُ بِمَا يَصِفُونَSorah Al-Mu'minoon ( The Believers ) Verse Number 96
Kinga maovu kwa kutenda yaliyo mema zaidi. Sisi tunajua wayasemayo.
وَقُل رَّبِّ أَعُوذُ بِكَ مِنْ هَمَزَاتِ الشَّيَاطِينِSorah Al-Mu'minoon ( The Believers ) Verse Number 97
Na sema: Mola wangu Mlezi! Najikinga kwako na wasiwasi wa mashet'ani.
وَأَعُوذُ بِكَ رَبِّ أَن يَحْضُرُونِSorah Al-Mu'minoon ( The Believers ) Verse Number 98
Na najikinga kwako, Mola wangu Mlezi, wasinikaribie.
حَتَّى إِذَا جَاءَ أَحَدَهُمُ الْمَوْتُ قَالَ رَبِّ ارْجِعُونِSorah Al-Mu'minoon ( The Believers ) Verse Number 99
Mpaka yanapo mfikia mmoja wao mauti, husema: Mola wangu Mlezi! Nirudishe.
لَعَلِّي أَعْمَلُ صَالِحًا فِيمَا تَرَكْتُ كَلاَّ إِنَّهَا كَلِمَةٌ هُوَ قَائِلُهَا وَمِن وَرَائِهِم بَرْزَخٌ إِلَى يَوْمِ يُبْعَثُونَSorah Al-Mu'minoon ( The Believers ) Verse Number 100
Ili nitende mema sasa badala ya yale niliyo yaacha. Wapi! Hii ni kauli aisemayo yeye tu. Na nyuma yao kipo kizuizi mpaka siku watapo fufuliwa.
فَإِذَا نُفِخَ فِي الصُّورِ فَلا أَنسَابَ بَيْنَهُمْ يَوْمَئِذٍ وَلا يَتَسَاءَلُونَSorah Al-Mu'minoon ( The Believers ) Verse Number 101
Basi litapo pulizwa baragumu hapo hautakuwapo ujamaa baina yao siku hiyo, wala hawataulizana.
فَمَن ثَقُلَتْ مَوَازِينُهُ فَأُولَئِكَ هُمُ الْمُفْلِحُونَSorah Al-Mu'minoon ( The Believers ) Verse Number 102
Ama wale ambao mizani zao zitakuwa nzito, hao ndio wenye kufanikiwa.
وَمَنْ خَفَّتْ مَوَازِينُهُ فَأُولَئِكَ الَّذِينَ خَسِرُوا أَنفُسَهُمْ فِي جَهَنَّمَ خَالِدُونَSorah Al-Mu'minoon ( The Believers ) Verse Number 103
Na wale ambao mizani zao zitakuwa nyepesi, hao ndio walio zitia khasarani nafsi zao, na katika Jahannamu watadumu.
تَلْفَحُ وُجُوهَهُمُ النَّارُ وَهُمْ فِيهَا كَالِحُونَSorah Al-Mu'minoon ( The Believers ) Verse Number 104
Moto utababua nyuso zao, nao watakuwa na nyuso zilizo kunjana.
أَلَمْ تَكُنْ آيَاتِي تُتْلَى عَلَيْكُمْ فَكُنتُم بِهَا تُكَذِّبُونَSorah Al-Mu'minoon ( The Believers ) Verse Number 105
Je! Hazikuwa Aya zangu mkisomewa, na nyinyi mkizikanusha?
قَالُوا رَبَّنَا غَلَبَتْ عَلَيْنَا شِقْوَتُنَا وَكُنَّا قَوْمًا ضَالِّينَSorah Al-Mu'minoon ( The Believers ) Verse Number 106
Mola wetu Mlezi! Tulizidiwa na uovu wetu na tukawa watu tulio potea.
رَبَّنَا أَخْرِجْنَا مِنْهَا فَإِنْ عُدْنَا فَإِنَّا ظَالِمُونَSorah Al-Mu'minoon ( The Believers ) Verse Number 107
Mola wetu Mlezi! Tutoe humu Motoni. Na tufanyapo tena basi kweli sisi ni wenye kudhulumu.
قَالَ اخْسَؤُوا فِيهَا وَلا تُكَلِّمُونِSorah Al-Mu'minoon ( The Believers ) Verse Number 108
Atasema Mwenyezi Mungu: Tokomeeni humo, wala msinisemeze.
إِنَّهُ كَانَ فَرِيقٌ مِّنْ عِبَادِي يَقُولُونَ رَبَّنَا آمَنَّا فَاغْفِرْ لَنَا وَارْحَمْنَا وَأَنتَ خَيْرُ الرَّاحِمِينَSorah Al-Mu'minoon ( The Believers ) Verse Number 109
Bila ya shaka lilikuwapo kundi katika waja wangu likisema: Mola wetu Mlezi! Tumeamini; basi tusamehe na uturehemu, nawe ndiwe Mbora wa wanao rehemu.
فَاتَّخَذْتُمُوهُمْ سِخْرِيًّا حَتَّى أَنسَوْكُمْ ذِكْرِي وَكُنتُم مِّنْهُمْ تَضْحَكُونَSorah Al-Mu'minoon ( The Believers ) Verse Number 110
Lakini nyinyi mliwakejeli hata wakakusahaulisheni kunikumbuka, na mlikuwa mkiwacheka.
إِنِّي جَزَيْتُهُمُ الْيَوْمَ بِمَا صَبَرُوا أَنَّهُمْ هُمُ الْفَائِزُونَSorah Al-Mu'minoon ( The Believers ) Verse Number 111
Hakika Mimi leo nimewalipa kwa vile walivyo subiri. Bila ya shaka hao ndio wenye kufuzu.
قَالَ كَمْ لَبِثْتُمْ فِي الأَرْضِ عَدَدَ سِنِينَSorah Al-Mu'minoon ( The Believers ) Verse Number 112
Atasema: Mlikaa muda gani katika ardhi kwa hisabu ya miaka?
قَالُوا لَبِثْنَا يَوْمًا أَوْ بَعْضَ يَوْمٍ فَاسْأَلْ الْعَادِّينَSorah Al-Mu'minoon ( The Believers ) Verse Number 113
Watasema: Tulikaa siku moja au sehemu ya siku. Basi waulize wanao weka hisabu.
قَالَ إِن لَّبِثْتُمْ إِلاَّ قَلِيلا لَّوْ أَنَّكُمْ كُنتُمْ تَعْلَمُونَSorah Al-Mu'minoon ( The Believers ) Verse Number 114
Atasema: Nyinyi hamkukaa huko duniani ila kidogo, laiti ingeli kuwa mnajua.
أَفَحَسِبْتُمْ أَنَّمَا خَلَقْنَاكُمْ عَبَثًا وَأَنَّكُمْ إِلَيْنَا لا تُرْجَعُونَSorah Al-Mu'minoon ( The Believers ) Verse Number 115
Je! Mlidhani ya kwamba tulikuumbeni bure na ya kwamba nyinyi kwetu hamtarudishwa?
فَتَعَالَى اللَّهُ الْمَلِكُ الْحَقُّ لا إِلَهَ إِلاَّ هُوَ رَبُّ الْعَرْشِ الْكَرِيمِSorah Al-Mu'minoon ( The Believers ) Verse Number 116
Ametukuka Mwenyezi Mungu, Mfalme wa Haki, hapana mungu ila Yeye, Mola Mlezi wa A'rshi Tukufu.
وَمَن يَدْعُ مَعَ اللَّهِ إِلَهًا آخَرَ لا بُرْهَانَ لَهُ بِهِ فَإِنَّمَا حِسَابُهُ عِندَ رَبِّهِ إِنَّهُ لا يُفْلِحُ الْكَافِرُونَSorah Al-Mu'minoon ( The Believers ) Verse Number 117
Na anaye muomba - pamoja na Mwenyezi Mungu - mungu mwenginewe hana ushahidi wa hili; basi bila ya shaka hisabu yake iko kwa Mola wake Mlezi. Kwa hakika makafiri hawafanikiwi.
وَقُل رَّبِّ اغْفِرْ وَارْحَمْ وَأَنتَ خَيْرُ الرَّاحِمِينَSorah Al-Mu'minoon ( The Believers ) Verse Number 118
Nawe sema: Mola wangu Mlezi! Samehe na urehemu nawe ni Mbora wa wanao rehemu.